sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» »Unlabelled » SEMINA MAALUMU YA WATUMISHI WOTE WA UHAMIAJI MKOA WA SHINYANGA



Na Mohab Dominick
Kahama
Nov 19, 2013.

WATUMISHI UHAMIAJI SHINYANGA WAPATA MAFUNZO YA MAADILI YA KAZI.

WATUMISHI  wa Serikali wametakiwa kuwa na utaratibu wa kutunza siri za Serikali pamoja na kusimamia misingi , sheria na taratibu zilizowekewa kwa lengo la kuleta ufanisi katika maeneo yao husika ya kazi.

Hayo yalibainishwa juzi na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Halmashauri ya Msalala Patrick Karangwa katika semina ya siku moja iliyojumuisha Wafanyakazi kutoka katika Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Shinyanga ilifanyika Mji Kahama

Kalangwa ambaye  alikuwa Mgeni Rasmi kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Kahama Benson Mpesya katika semina hiyo alisema kuwa kwa sasa ni wajibu wa Watumishi wa umma kufuata sheria na taratibu ili utendaji wa kazi uweze kufanyika kwa ufanisi.

Aidha Kalangwa alisema kuwa watumishi hao wa Serikali hususani wa Idara ua uhamiaji lazima wajenge imani ya kuaminika na wateja wao wanaowatumikia hali ambayo itaepusha malalamiko katika idara husika.

Pia aliendelea kusema kusema kuwa kama mfanyakazi atakuwa anafanya vizuri katika utendeji wake wa kazi hata nafasi zinapotokea za kwenda kujiendeleza atakuwa wa kwanza kuchaguliwa kwa ajili jitihada alizozionyesha wakati wa kazi yake.

Awali Naibu Kamishna wa Uhamiaji Mkoa wa Shinyanga AnnaMaria Yondani alisema kuwa lengo la Semina hiyo ni kukumbushana juu ya maadili ya Utumishi wa umma pamoja na utunzaji wa Nyaraka mbalimbali za Serikali.

Yondani aliendelea kusema kuwa Semina hizo zinazofanywa na Idara yake ni za mara kwa mara ili kuwakumbusha watumishi wa Idara hiyo ya Uhamiaji juu ya Maadili ya kazi pamoja na mambo mengine yanayohusu Idara hiyo.

Hata hivyo alisema kuwa Semona hiyo inawajumuisha Watumishi wa iadara ya Uhamiaji kutoka katika ofisi za Shinyanga, Isaka pamoja na Kahama na kuongeza kuwa ofisi yake tayari imeunda kamati kwa ajili kusimamia nidhamu pamoja na mafunzo kama hayo kwa ujumla.

mwisho

 MGENI RASM MKURUNGEZI WA HALMASHAURI YA MSALALA PATRICK KARANGWA,KWA NIAMBA YA MKUU WA WILAYA YA KAHAMA KATIKA SEMINA YA MADILI YA UONGOZI MJINI KAHAMA. 
 BAADHI YA WATUMISHI WA IDARA YA UHAMIAJI MKOA WA SHINYANGA NA KAHAMA WAKISIKILIZA MGENI RASMI MKURUNGEZI WA MSALALA HAYUPO PICHANI
 BAADHI YA WATUMISHI WA IDARA YA UHAMIAJI WA WILAYA YA KAHAMA NA MGENI RASMI PATRICK KARANGWA MWENYE SHARTI NYEUPE NA MWISHO KULIA ALIKAA NI KAMISHA WA UHAMIAJI WA MKOA WA SHINYANGA ANNAMARIA YONDANI

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply