sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» »Unlabelled » .SLAA NA MNYIKA WAZIDI KUIBOMOA KAMBI YA ZITO. .CHOPA DR SLAA YA POTEA NJIA KATA YA UBAGWE KAHAMA



 Na 
 CHOPA YA CHADEMA IKIWASILI KATIKA VIWANJA  CHA MCHEZO CHA MPIRA HALMASHAURI YA MJI WA KAHAMA KWA AJILI YA KAMPENI YA PAMOJA DAIMA 
 BAADHI YA WAKAZI WA KAHAMA WAKIMSIKILIZA KATIBU MKUU WA CHADEMA DR WIILBROD SLAA AKIWAHUTUMBIA WAKAZI WA KAHAMA KATIKA VIWANJA YA HALMASHAURI YA MJI WA KAHAMA
 KATIBU MKUU WA CHADEMA DR WILLBROD SLAA AKIWAHUTUMBIA WAFASI WA CHADEMA KATIKA VIWANJA VYA MICHEZO KAHAMA KATIKA KAMPENI YAO YA PAMOJA DAIMA
 PIA MABANGO KAMA HAYA YALIKUWEPO
 UMATI MKUBWA WA WANACHINI WAKIFURAHI HOTUBA YA KATIBU MKUU WA CHADEMA JANA MJINI KAHAMA
 HII NDIYO CHOPA YA CHADEMA IKIWA IMESIMAMA BAADA YA KUTUA KATIKA VIWANJA VYA MICHEZO KAHAMA

 BAADHI  VIONGOZI WA KITAIFA WA CHAMA CHA DEMOKRASIA NA  MAENDELEO (CHADEMA)KATIKA JUKWAA KABLA YA KUANZA KWA MKUTANO WA PAMOJA DAIMA JANA MJINI KAHAMA
  Jan 29, 2014.


KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Wilbrod Slaa na Katibu Mwenezi wake John Mnyika juzi wamemkataa Diwani wa Kata ya Majengo mjini hapa kupitia Chama chao na kusema kuwa ni msaliti huku akituhumiwa na chama cha Mapunduzi katika kukihujumu cha hicho.

Hayo yalisemwa juzi na Katika mkutano wa Hadhara na katibu Mwenezi wa CHADEMA John Mnyika wakati akiwahutubia wakazi wa mji wa Kahama katika moja ya mikutano ya chama hicho ijulikanayo kama operesheni  pamoja daima.

Mnyika alisema kuwa katika chama chao hawatakubali kuwa na watendaji wasaliti na kwa sasa wapo katika kazi ya kuwaondo watu kama Diwani huyo ambaye walimwita ni msaliti mkubwa wa chama hicho na alipaswa kuondolewa kabisa.

Mnyika alisema kuwa moja sababu zilizofanya Diwani huyo kuondolewa katika chama hicho ni madai ya kuwa alishiriki katika kufanikisha Chama hicho cha Demokrasia na maendeleo hakipeleki mgombea udiwani katika kata ya Ubagwe wilayani kahama  ambapo uchaguzi wa udiwani unatajiwa kurudiwa kutoka na aliyekuwa Diwani wa kata hiyo Robert Mndula kufariki dunia mwaka jana.

Pia sababu nyingine ni madai ya kuwa alikuwa akizunguka mitaani mitaani na kuwaambia watu kuwa baadhi ya Viongozi wa CHADEMA walitoa kiasi cha shilingi milioni tano ili kuwashinikiza wananchi wahudhurie katika mkutano huo ulifanyika juzi mjini Kahama.
“Mimi ndie katibu Mwenezi wa chama cha Demokrasia na Maendeleo hapa nchini na Bobson ni Katibu  Mwenezi wa Wilaya ya Kahama je, Wananchi unaniruhusu niondoke Diwani huyo”, Alihoji Mnyika Katibu Mwenezi wa Chadema Taifa.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Majengo Bobson Wambura akiongea na Gazeti la nipashe akiwa Jijini Mwanza kwa njia ya simu ya kiganjani kuhusu tuhuma hizo alisema kuwa tuhuma hizo sii za kweli na wameamua kufanya hivyo kwa ajili msimamo wangu Zitto Kabwe.

“Mimi bwana Mwandishi Zitto Kabwe ni rafiki yangu iwe ndani ya chama au nje ya chama na nipo tayari kwa lolote watakaloamua wenyewe mimi chadema sio yangu kwani hapo zamani nilikuwa naishi kwa udiwani au chama?, Alisema Bobson Wambura Diwani wa kata ya majengo.

Hata hivyo msafara huo ambao ulikuwa ukiongozwa na John Mnyika pamoja na Dr, Slaa haukufanikiwa kufika katika eneo la Ubagwe  ambapo uchaguzi mdogo wa kiti cha udiwani unatarajiwa kufanyika kutoka chopa walikuwa wakitumia kupotea njia na kutua sehemu nyingine na hivyo kufanya safari yao kuihairisha.

Mwisho.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply