sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» »Unlabelled » WAZEE KAHAMA WAKATAA MWALIKO WA HALMASHAURI. WASISITIZA MADIWANI AMBAO HAWAKWENDA MBEYA KUJIFUNZA WARUDISHE FEDHA ZA WANANCHI




Na  Mohab Dominick
Kahama
May 21, 2014.

UMOJA wa Wazee Wilaya ya Kahama Mkoani Shinyanga (UWAKA) juzi ulikataa Mwaliko wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Mji wa Kahama kutokana kile wachosema kuwa mpaka Madiwani wanne ambao hawakwenda katika ziara ya kujifunza katika Jiji la Mbeya kurudisha fedha za Wananchi walizochukua kiasi cha Milioni 1.9 na kisha kukwepa safari hiyo

Katika barua yao kwa vyombo vya habari yenye kumb Namba UWAKA/KHM/2014/43 kupitia kwa katibu wa umoja huo Paul Ntelya wazee hao walikataa Mwaliko huo ulitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Kahama kuhudhuria kikao kwa pia ya Halmashauri hiyo haiutambui umoja  huo.
Ntelya alisema kuwa Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Machibya Judulamabambasi alitangaza kutoutambua umoja huo kupitia katika vyombo vya Habari zikiwemo Radio Station hali ambayo walisema ni kama kitendo cha kuwadhalilisha katika jamii.

“Hatuoni Mantinki ya kukubali Mwaliko huo labda kama Mwenyewkiti wa Halmashauri ya Mji huo abadilishe uamuzi wake kupitia katika vyomba vya habari vilevile  kama alifanya mwanzo ili dunia yote ipate kujua”, Alisema Paul Ntelya Katibu wa Umoja wa Wazee Wilayani Kahama.

Ntelya alisema pamoja na kutokubali Mwaliko huo bado umoja wa Wazee Wilayani hapa unasisitiza kuwa Madiwani Mabubu Musa Mabubu, James Mlekwa, Bobson Wambura na Josephine Balanoga waliopewa fedha za posho kwa ajili ya safari ya kwenda katika Jiji la Mbeya kujifunza na kutoenda wazirejeshe fedha hizo katika muda wa suku 30 kinyume cha hapo umoja huo utawafikisha mahakamani.
“fedha za Halmashauri ni Kodi za Wananchi na sisi Wazee moja ya Wananchi na tuna uwezo wa kuhoji juu ya matumizi ya fedha za zinazotokana na Walipakodi na hizo fedha walizotumia katika safari yao ya siku tano ni kwetu”,Aliongeza Paul Ntelya Katibu wa Umoja wa Wazee Kahama.

Katibu huyo wa Wazee aliendelea kusema kuwa kitendo cha Madiwani hao kuchukua posho kiasi cha shilingi 480,000 kila mmoja na kuhairisha safari ni kama kitendo cha wizi cha kuwaibia Wananchi fedha zao za kodi wanazochangia kwa Serikali.

Baadhi ya Madiwani walionekana wakinunua Mabati na vifaa vingine vua ujenzi baada ya kuchukia kiasi hicho cha fedha hali ambayo baadhi ya Wananchi walionekana kukerwa na kitendo hicho wakiwemo Wazee na hivyo kufanya kuhoji juu ya Madiwani hao kukwepa safari hiyo na kubaki huku wangine wakiishia katikati ya safari.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Kahama Machibya Jidulamabambasi alipohojiwa juu ya suala hilo alisema Halmashauri yake bado inalifanyia kazi suala hilo lakini kimsingi Madiwani wake hawawajibiki kwa Wazee

Mwisho.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply