sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» »Unlabelled » WAKANDARASI WATAKIWA KUMALIZA KAZI ZA MIRADI YA MAJI KWA WAKATI



  
Na Mohab Dominick
       Kahama
      March 24,2014.


SERIKALI imewataka Wakandarasi wanaojenga miradi mbalimbali  ya maji Mkoani Shinyanga wametakiwa kumaliza kazi za miradi hiyo waliopewa na Halmashauri husika  kwa wakati  kwa mujibu wa mikataba yao ya kazi inavyoonyesha kumaliza kazi hiyo.

Hayo yalisemwa juzi na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Ally Rufunga katika kilele cha Wiki ya maji ambayo ambao kimkoa ilifanyika katika kijiji cha Kagongwa Wilayani Kahama na kusisitiza kuwa wakandarasi wengi wamekuwa wakikwamisha miradi hiyo.

Rufunga alisema kuwa kama Wakandarasi wangekuwa wakimaliza kazi mapema ya kujenga miradi ya maji basi Wananchi wangeweza kufaidika na michango yao ambao wamekuwa wakichanga katika kufanikisha huduma hiyo muhimu.

Pia Mkuu huyo wa Mkoa wa Shinyanga aliwataka wananchi wanapopata miradi ya maji katika maeneo yao kujitahidi kuiunga mkono Serikali kwa kutoa ushirkiano katika suala zima la kuchangia miradi hiyo ili iweze kuwanufaisha watu wa maeneo hayo hasa maeneo ya Vijijini.

Aidha katika kilele hicho cha Wiki ya maji Mkuu huyo wa Mkoa wa Shinyanga alifungua mradi wa maji wa Kagongwa Iponya uliosimamiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Kahama wenye thamani ya shilingi milioni 432.4 ambao utahudumia jumla ya wakazi 11,293 wa vijiji hivyo pamoja na Tanki lenye uwezo wa kuchukua lita zipatazo 50,000 za maji.

Rufunga alisema kuwa kupata maji kwa wakazi wa Kagongwa na Iponya Wilayani Kahama kuwa ni mwanzo tuu wakisubiri mradi mkubwa kule wa ziwa ziwa Victoria ambao utapita katika Kata hiyo ukipeleka maji katika maeneo ya Isaka, Tinde mpaka Tabora ambao upo katika upembuzi yakinifu kwa sasa ukisubiri  bajeti ijayo kwa ajili ya kuanza kwa ujenzi wa mradi huo.

Awali akisoma Risala kwa naiba ya Halmashauri ya Wilaya Mhandishi Charles Pambe alisema kuwa mpaka kufikia hivi sasa nia asilimia 63 ya Wakazi wa Halmashauri ya mji wa Kahama ndio wanaopata huduma ya maji safi na salama na kuongeza kuwa kiwango hicho bado ni kidogo kulinganishwa na kile cha Taifa.

Pambe alisema kuwa kwa upande wa Changamoto zinazikabili Idara yake ya maji katika Mji wa Kahama na pamoja maeneo ya Vijijini kitendo cha Wananchi kutoshiriki katika kuchangia huduma za maji hali ambayo inafanya sehemu nyingi za Vijijini kutokuwa na maji kwa muda mrefu.

 MKUU WA MKOA WA SHINYANGA ALLY  NASSOR RUFUNGA AKIFUNGUA MRADI WA TANKI LA  MAJI KATIKA KIJIJI CHA KAGONGWA  KATIKA SIKU YA MAJI DUNIAN
 MKUU WA MKOA WA SHINYANGA ALLY NASSOR RUFUNGA AKITWISHA NDOO YA MAJI MJUMBE WA KAMATI YA MAJI ANNASTAZIA MAYAI WAKATI WA UZINDUZI WA MRADI WA MAJI KATIKA KIJIJI CHA KAGONGWA MRADI HUU WA MAJI UMEGHARIMU JUMLA YA SHILINGI MILIONI 432,4 AMBAO UTAHUDUMIA WAKAZI 11,293 PAMOJA NA TANKI LA MAJI LENYE UWEZO WA LITA 50,000
 MKUU WA MKOA WA SHINYANGA ALLY RUFUNGA AKIWA NA MWENYEKITI WA CCM  WA MKOA WA SHINYANGA KHAMISI MGEJA AKIONYESHA JINSI ILANI YA SERIKALI YA CCM INAVYOTIMIZA WAJIBU WAKE WA WANANCHI KWA KULETA HUDUMA YA MAJI SIKU YA MAJI DUNIA KATIKA KIJIJI CHA KAGONGWA
 MKUU WA MKOA WA SHINYANGA AFUNGUA MRADI WA MAJI  KAGONGWA KATIKA SIKU YA MAJI DUNIANI KULIA NI MWENYEKITI WA CCM MKOA WA SHINYANGA KHAMIS MGEJA
 MKUU WA MKOA WA SHINYANGA ALLY NASSOR RUFUNGA AKIFUNGUA KITAMBAA KATIKA TANKI LA MAJI KAGONGWA
 MKUU WA MKOA WA SHINYANGA ALLY NASSOR RUFUNGA KUONA JINSI MRADI WA MAJI KATIKA KIJIJI CHA KAGONGWA DUNIANI
Wanafunzi wa shule ya msingi kishima( AB )Wakiimba wimbo wa siku ya maji Dunia katika kijiji cha kagongwa ambayo yalifanyika kimkoa wilaya kahama  picha zote na mohab Dominick( kahama)

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply