Na
Mohab Dominick
Kahama
March 24,2014.
SERIKALI
imewataka Wakandarasi wanaojenga miradi mbalimbali ya maji Mkoani
Shinyanga wametakiwa kumaliza kazi za miradi hiyo waliopewa na Halmashauri
husika kwa wakati kwa mujibu wa mikataba yao ya kazi inavyoonyesha
kumaliza kazi hiyo.
Hayo
yalisemwa juzi na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Ally Rufunga katika kilele cha Wiki
ya maji ambayo ambao kimkoa ilifanyika katika kijiji cha Kagongwa Wilayani
Kahama na kusisitiza kuwa wakandarasi wengi wamekuwa wakikwamisha miradi hiyo.
Rufunga
alisema kuwa kama Wakandarasi wangekuwa wakimaliza kazi mapema ya kujenga
miradi ya maji basi Wananchi wangeweza kufaidika na michango yao ambao wamekuwa
wakichanga katika kufanikisha huduma hiyo muhimu.
Pia
Mkuu huyo wa Mkoa wa Shinyanga aliwataka wananchi wanapopata miradi ya maji
katika maeneo yao kujitahidi kuiunga mkono Serikali kwa kutoa ushirkiano katika
suala zima la kuchangia miradi hiyo ili iweze kuwanufaisha watu wa maeneo hayo
hasa maeneo ya Vijijini.
Aidha
katika kilele hicho cha Wiki ya maji Mkuu huyo wa Mkoa wa Shinyanga alifungua
mradi wa maji wa Kagongwa Iponya uliosimamiwa na Halmashauri ya Wilaya ya
Kahama wenye thamani ya shilingi milioni 432.4 ambao utahudumia jumla ya wakazi
11,293 wa vijiji hivyo pamoja na Tanki lenye uwezo wa kuchukua lita zipatazo
50,000 za maji.
Rufunga
alisema kuwa kupata maji kwa wakazi wa Kagongwa na Iponya Wilayani Kahama kuwa
ni mwanzo tuu wakisubiri mradi mkubwa kule wa ziwa ziwa Victoria ambao utapita
katika Kata hiyo ukipeleka maji katika maeneo ya Isaka, Tinde mpaka Tabora
ambao upo katika upembuzi yakinifu kwa sasa ukisubiri bajeti ijayo kwa
ajili ya kuanza kwa ujenzi wa mradi huo.
Awali
akisoma Risala kwa naiba ya Halmashauri ya Wilaya Mhandishi Charles Pambe
alisema kuwa mpaka kufikia hivi sasa nia asilimia 63 ya Wakazi wa Halmashauri
ya mji wa Kahama ndio wanaopata huduma ya maji safi na salama na kuongeza kuwa
kiwango hicho bado ni kidogo kulinganishwa na kile cha Taifa.
Pambe
alisema kuwa kwa upande wa Changamoto zinazikabili Idara yake ya maji katika
Mji wa Kahama na pamoja maeneo ya Vijijini kitendo cha Wananchi kutoshiriki
katika kuchangia huduma za maji hali ambayo inafanya sehemu nyingi za Vijijini
kutokuwa na maji kwa muda mrefu.
MKUU WA MKOA WA SHINYANGA ALLY NASSOR RUFUNGA AKITWISHA NDOO YA MAJI MJUMBE WA KAMATI YA MAJI ANNASTAZIA MAYAI WAKATI WA UZINDUZI WA MRADI WA MAJI KATIKA KIJIJI CHA KAGONGWA MRADI HUU WA MAJI UMEGHARIMU JUMLA YA SHILINGI MILIONI 432,4 AMBAO UTAHUDUMIA WAKAZI 11,293 PAMOJA NA TANKI LA MAJI LENYE UWEZO WA LITA 50,000
MKUU WA MKOA WA SHINYANGA ALLY RUFUNGA AKIWA NA MWENYEKITI WA CCM WA MKOA WA SHINYANGA KHAMISI MGEJA AKIONYESHA JINSI ILANI YA SERIKALI YA CCM INAVYOTIMIZA WAJIBU WAKE WA WANANCHI KWA KULETA HUDUMA YA MAJI SIKU YA MAJI DUNIA KATIKA KIJIJI CHA KAGONGWA
MKUU WA MKOA WA SHINYANGA AFUNGUA MRADI WA MAJI KAGONGWA KATIKA SIKU YA MAJI DUNIANI KULIA NI MWENYEKITI WA CCM MKOA WA SHINYANGA KHAMIS MGEJA
MKUU WA MKOA WA SHINYANGA ALLY NASSOR RUFUNGA AKIFUNGUA KITAMBAA KATIKA TANKI LA MAJI KAGONGWA
MKUU WA MKOA WA SHINYANGA ALLY NASSOR RUFUNGA KUONA JINSI MRADI WA MAJI KATIKA KIJIJI CHA KAGONGWA DUNIANI
Wanafunzi wa shule ya msingi kishima( AB )Wakiimba wimbo wa siku ya maji Dunia katika kijiji cha kagongwa ambayo yalifanyika kimkoa wilaya kahama picha zote na mohab Dominick( kahama)
No comments: