sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» » » IDARA YA UHAMIAJI KAHAMA YAFANIKIWA KUWARUDISHA WAHAMIAJI HARAMU 31 NCHI KWAO

 Afisa Uhamiaji wa wilaya ya kahama akichukuwa maelenzo kwa wahamiaji Haramu katika ofisi za uhamiaji wilayani kahama.
 Baadhi ya wahamiaji haramu wakiwa chini ya ulinzi baada ya kutiwa baroni mjini kahama.
 Wahamiaji harama wakiwa katika ofisi ya uhamiaji kwa mahojiano
 Afisa uhamiaji wilaya ya kahamakamishina zakaria missana akiongea na vyombo vya habari mbali mbali ofisini kwake jana juu ya wahamiaji haramu.wanaongia katika wilaya ya kahama mkoa wa shinyanga .
 Muandishi wa habari wa TBC  Taifa ,Greyson kakuru akichukuwa taarifa kwa wahamiaji harama katika ofisi ya uhamiaji wilayani kahama.
 Kamishina wa uhamiaji Zakaria missana akifanya mahojiano na baadhi ya wahamiaji haramu ofisi kwake.



 Baadhi ya wahamiaji haramu wakiwa chini ya ulinzi katika ofisi za uhamiaji wilayani kahama mkoani shinyanga.
Kamishina wa Uhamiaji wilaya ya kahama Zakaria Missana akionyesha kidole moja ya wahamiaji haramu ofisini kwake.

KAHAMA.
KUANZIA mwezi wa kwanza hadi mwezi nne 2015 idara ya uhamiaji wilayani kahama mkoani shinyanga imefanikiwa kuwarudisha nchini mwao wahamiaji haramu 31 kutoka nchi mbalimbali nchini walioingia nchin Tanzania bila kufuata utaratibu,sheria na kanuni za kuingia nchi.

Hayo yalibainishwa jana na Ofisa uhamiaji wa wilaya ya kahama Zakaria Missana wakati alipokuwa akizungumza na wandishi wa habari ofisini kwakwe, ambapo alisema kuwa idara ya uhamiaji inafanya kazi kwa kuzingatia sheria na taaratibu za nchi.

Alisema kuwa raia waliorudishwa nchi mwao walikuwa raia kutoka nchi mbalimbali,ambapo nchi hizo ni nchi ya Congo alikuwa raia mmoja(1), Burundi walikuwa raia 22,Uganda walikuwa raia 2, huku Kenya walikuwa 3, pamoja na Rwanda walikuwa raia 3. 

“Tunafanya kazi vema kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama bila kuwasahau wananchi katika maeneo mbalimbali ya mji wa kahama na mkoani ili kukamilisha shughuli nzima lawatu kuingia nchi kiholela bila kufuata utaratibu ikiwa ni pamoja na kulikomesha zoezi la kuingia nchini Tanzania bila kuwa na kibari” alisema Ofisa Missana.

Hata hivyo Missana alisema kunabaadhi ya raia kutoa nchi ya Burundi na Rwanda walifikishwa mahakamani kwakosa la kukaidi amri ya serikali yakutorudi nchini mwao,ambapo  Audresile ni raia wa nchi ya Burundi alikamatwa tarehe 27,04 kwakosa lakuingia nchi bila kibari na kuweka makazi huku akidanganya kuwa anatoka ngara.

Alisema kuwa Ndaisenga Nuru ni raia wa nchi ya Rwanda alikamatwa kwa mara ya pili Tarehe 25 mwezi 4 mwaka 2015 kwakosa la kuingia nchini na kuweka makazi bila kufuata sheria,taaratibu na kanuni za kukaa nchini huku akidanganya kuwa ni raia kutoka Kigoma wilaya ya kasulu.

Aidha missana alisema kuwa idara ya uhamiaji imekuwa ikifanya kazi kwa ushirikiano na wananchi ambapo Erick Venas Peter Raia wanchi ya Jamhuri ya Burundi alifukuzwa nchini Tanzania kwakosa la kuingia nchini bila kibari hivyo na kukaidi amri ya serikali ambapo aliendelea kuweka makazi, na alikamatwa na kufikishwa mahakamani nakutozwa faini ya shilling 3000 au kwenda jela miezi 6.

Nae Jokson Peter raia wanchi ya Burundi alikamatwa tarehe 27 mwezi 4 mwaka huu nakufikishwa mahakama ya wilaya ya kahama kwakosa la kukaidi ya amri ya serikali ya kuondoka nchi na kuhukumiwa kifungo cha kwenda jela miezi 30, ambapo missana alisema jokson Peter alifukuzwa nchini 17/03/2009, hivyo nakukatwa 27/04/2015.

“Tumekuwa tukifanya ukaguzi mara kwa mara katika maeneo mbalimbali,na tareh 4/05 mwaka huu tulikagua katika gesti ya CDT na tulikuta wageni kutoka nchi mbalimbali  na walikuwa raia 27 katika gesti hiyo,hivyo basi Wakongo walikuwa 10,waganda 2,Burundi 7,Rwanda 2 na Naigeria 1,nawageni wote walikuwa na vibali halali vya kuingia na kutoka nchini” alisema ofisa Missana.

“Missana aliendelea kusema kuwa”Sisi hatukatazi wageni kuingia nchini,bali sisi tunawakataa wale wanaoingia kiholela bila kufuata utaratibu na sheria za nchi,na tunatambua wazi kuwa kahama ni kitovu cha biashara na kahama napokea wageni kutoka nchi za Rwanda,Kongo,Burundi,Ungada na Kenya na wote wanakuja kuchua bidhaa kahama,sisi kama idara ya uhamiaji tunawaomba wafute sheria za kuingia nchin”
.
Katika hatua nyingine missana alisema kuwa kutokana na kauli ya jumuia ya afrika mashariki imelenga kuhamasisha wanajumuia watembeleane kwa kufuata taaratibu za uingiaji na utokaji wa nchi husika kwa kuwa na vibari halali na sio kutembelea kiholela bila kufuata utaaratibu.
Mwisho 

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply