sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» » CHADEMA WAIPASUA CCM SHINYANGA, WAMCHOMOA KATIBU MWENEZI WILAYA, DIWANI VITI MAALUM

CHADEMA WAIPASUA CCM SHINYANGA, WAMCHOMOA KATIBU MWENEZI WILAYA, DIWANI VITI MAALUM.



Charles shigino akiongea na waandishi wa habari mjini shinyanga
 
katibu wa  muenezi wa ccm wilaya ya shinyanga charles shigino 

KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida, katibu wa siasa na uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Shinyanga mjini, Charles Shigino ametangaza rasmi kukihama chama chake cha CCM na kujiunga na CHADEMA.
  
Shigino ambaye pia alikuwa mmoja wa wana CCM walioomba kugombea ubunge kwa tiketi ya CCM jimbo la Shinyanga  ametangaza uamuzi wake huo mbele ya waandishi wa habari na kueleza kuwa moja ya sababu iliyosababisha achukue uamuzi huo ni kuchoshwa na mizengwe iliyomo ndani ya chama hicho.
Alisema ndani ya Chama cha Mapinduzi mambo mengi yamekuwa hayaendeshwi kwa mujibu wa katiba na taratibu za chama na badala yake kufuata matakwa ya watu binafsi ikiwemo kukithiri kwa vitendo vya rushwa hali inayokidhalilisha chama hicho.
“Mimi ni miongoni mwa wana CCM tulioomba kugombea nafasi ya ubunge ndani ya Chama chetu, lakini mizengwe inayoendelea inayofanywa na baadhi ya viongozi wa CCM nimeona hata kama nikishinda kura za maoni kuna mipango ya jina  langu kukatwa kutokana na chuki binafsi,”
“Pamoja na kuwa kiongozi wa kiwilaya lakini nimekuwa sishirikishwi kwenye vikao vingi vya kikatiba, mara nyingi ninapotetea haki za wananchi wetu naelezwa eti mimi ni msaliti, sasa nimechoka na nimeamua kubwaga manyanga na nimetangaza kujiunga na CHADEMA,” alieleza Shigino.
Kaimu katibu wa CHADEMA wilayani Shinyanga, George Kitalama amethibitisha kupokelewa rasmi kwa mwenezi huyo wa CCM na kwamba alikabidhiwa kadi ya CHADEMA juzi pamoja na aliyekuwa diwani wa viti maalum (CCM) kata Ibadakuli Zimila Kalwani.
Kitalama alisema ndani ya kipindi cha wiki nzima CHADEMA imepokea zaidi ya wanachama 400 kutoka CCM waliojiunga na chama hicho na kwamba hali hiyo inatokana na wana CCM hao kuchoshwa na mfumo mbovu uliomo ndani ya chama hicho.
“Ni kweli jana tumempokea rasmi katibu mwenezi wa CCM wilaya ya Shinyanga mjini tangu jana (juzi), na siyo yeye tu kwa siku mbili za juzi na jana tumepokea wana CCM 36 na mpaka sasa tuna zaidi ya wanachama 400 waliojiunga na CHADEMA wakitokea CCM, ni hatua nzuri kwetu wakati tukielekea kwenye uchaguzi mkuu,” alieleza Kitalama.
Kwa upande wake mwenyekiti wa CCM wilaya ya Shinyanga mjini, Kanali mstaafu Tajiri Maulid alisema hakuwa na taarifa juu ya mwenezi wake kuhamia CHADEMA na kwamba ofisi yake pia haijapata taarifa rasmi juu ya tukio hilo.
“Sina taarifa kama kweli huyo bwana amekimbilia CHADEMA, ndiyo kwanza nasikia kutoka kwako, na kama ni kweli itakuwa nafuu kwetu, maana alikuwa mzigo, tunashukuru kwa kuondoka kwake, na ndiyo maana leo hii (jana) hakuongozana na wagombea wenzake kwenye mikutano ya kuomba kura kwa wana CCM kwa ajili ya kura za maoni,” alieleza Kanali Maulidi.
Kwa kipindi kirefu Shigino alikuwa haelewani na viongozi wenzake ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ambapo aliwahi kusimamishwa uongozi kwa madai ya kukiuka kanuni za chama kutokana na kitendo chake cha kuwatetea wafanyabiashara wadogo (machinga) waache kufukuzwa ovyo mitaani.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply