headlines

    9:53

sponsor

sponsor

Slider

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» » » eshi La Polisi Laua Watu 6 Jijijini Mwanza…….Ni Majambazi Hatari Yaliyokuwa Yametoroka Kibiti Na Kuingia Mwanza
 Mohab Dominic

 Majambazi sita wameuawa kwa kupigwa risasi sehemu mbalimbali za miili yao na Jeshi la Polisi baada ya kutokea majibizano ya risasi kati ya polisi na majambazi hao na kupatikana silaha moja aina ya AK 47 na nyingine nne zilizotengenezwa kienyeji.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, DCP Ahmed Msangi amesema tukio hilo limetokea usiku wa Julai 8, 2017,  katika mtaa wa Fumagila mashariki kata ya Igoma wilaya ya Ngamagana mkoani Mwanza baada ya kupokea taarifa kwa kwamba baadhi ya watu wanaofanya uhalifu katika mkoa wa Pwani wilaya ya Kibiti na Rufiji wamekimbilia mkoani humo wakijipanga kutengeneza vikundi vya kufanya uhalifu.
Kamanda Msangi amesema katika ufuatiliaji walifanikiwa kumkamata mtuhumiwa mmoja ambaye katika mahojiano alikiri kuhusika na tukio la unyang’anyi kwa kutumia silaha, kisha alitoa ushirikiano kwa askari ambapo aliwapeleka hadi eneo la Fumagila ambapo alidai wenzake wamejificha eneo hilo, ghafla majambazi hao walikurupuka na kuanza kuwarushia askari polisi risasi.
Aidha, kutokana na umahiri wa askari hao waliweza kujibu mashambulizi na kufanikiwa kuwauwa majambazi sita huku wengine wawili wakifanikiwa kutoroka eneo la tukio lakini polisi walifanikiwa kukamata silaha kadhaa na vitu vingine.
Pamoja na hayo, DCP Msangi amesema hakuna askari aliyejeruhiwa kwa risasi wala kupoteza maisha katika tukio hilo huku akisisitiza kuwa ufuatiliaji wa kusaka na kuwatia nguvuni waliotoroka bado unaendelea.
Shuhuda wa tukio hilo, ambaye ni diwani wa Kata ya Kishili iliyo jirani na kata hiyo, Sospeter Ndumi amesema kurushiana risasi baina ya watu hao na polisi kulianza usiku wa manane hadi majira ya jana asubuhi.
Amesema katika majibizano hayo polisi walifanikiwa kuwaua watu hao na kukamata silaha mbalimbali za kivita walizokuwa wanazitumia.
Katika mtaa huo huo ndipo lilipotokea tukio la Desemba 3 mwaka jana ambapo polisi waliwakamata watoto 11 wenye umri unaokadiriwa kuwa na miaka sita hadi 14 baada ya kuizingira nyumba moja kwa lengo la kuwakamata watu waliowahisi kuwa majambazi.
Mmoja kati ya watu watatu waliokutwa kwenye nyumba hiyo alikimbia baada ya kuwarushia polisi bumu la mkono, kabla ya polisi kuwadhibiti waliosalia kwa kushirikiana na wananchi wa mtaa huo.
Kadhalika katika tukio hilo, watu watatu waliosadikiwa kuwa ni majambazi waliuawa na bunduki mbili aina ya SMG na AK47, magazine saba, bastola moja na risasi 183 vilikamatwa na polisi.
Baada ya polisi kuondoka katika eneo hilo, wananchi waliiteketeza nyumba hiyo kwa moto.

«
Next
WAZIRI MKUU ATEMBELEA MRADI WA KINYEREZI II   WAZIRI MKUU ATEMBELEA MRADI WA KINYEREZI II   WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametembelea mradi ya kuzalisha umeme wa Kinyerezi II na kusema kwamba ameridhishwa na maendeleo ya ujenzi wake. Amesema hayo jana (Jumamosi, Julai 08, 2017) alipotembelea mradi huo wa kuzalisha umeme kwa kutumia gesi asilia unaojengwa eneo la Kinyerezi jijini Dar es Salaam. Waziri Mkuu alisema kukamilika kwa mradi huo kutaliwezesha Taifa kuwa na umeme wa uhakika, utakaowezesha kuendesha viwanda. Alisema mkakati wa Serikali ni kuongeza kiwango cha uzalishaji wa umeme ili Watanzania wapate umeme mwingi utakaosambazwa hadi vijijini kwa gharama nafuu. “Tunataka tupate umeme wa kutosha ili viwanda vitakavyojengwa viwe na nishati ya uhakika na ya gharama nafuu. Ni wajibu wetu kuendelea kuimarisha utekelezaji wa miradi hii.” Alisema. Naye, Meneja wa Mradi wa kuzalisha umeme wa Kinyerezi, Mhandisi Stephen Manda alisema gharama za mradi wa Kinyerezi II ni dola milioni 344. Meneja huyo alisema tayari mradi huo umefikia asilimia 66.32 ya ujenzi wake na sasa wako katika hatua mbalimbali za kukamilisha, ikiwemo ujenzi wa misingi ya mitambo na jengo la kuendeshea mitambo. “Pia tunaendelea na ujenzi wa nguzo za kupokelea laini ya msongo wa kilovoti 220 kutoka Kinyerezi I hadi Kinyerezi II, ambapo mtambo wa kwanza wa megawati 30 utawashwa ifikapo Desemba 2017 na kila mwezi tutaingiza megawati 30 katika gridi ya Taifa.” Alisema miradi iliyoko katika eneo hilo ambayo iko katika hatua mbalimbali za utekelezaji ni Kinyerezi 1 (150MW), Kinyerezi I Extension (185MW ) na Kinyerezi II (240MW). Mhandisi Manda aliongeza kuwa mradi wa Kinyerezi 1 (150MW) ulikamilika Machi 2015 na miradi mwili ya Kinyerezi 1-extension na Kinyerezi II inatarajiwa kukamilika mwaka 2018. Mhandisi Manda alisema miradi mingine inayotarajiwa kujengwa katika eneo hilo ni wa Kinyerezi III (600 MW) na Kinyerezi IV utakaozalisha (450 MW). Awali Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Bi. Sophia Mjema ambaye alimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Paul Makonda alisema mradi huo umewanufaisha wananchi wengi wa eneo hilo. Alisema hadi sasa wananchi 100 wa eneo la Kinyerezi wameajiriwa katika miradi hiyo ambapo ni sawa na asilimia 40 ya watumishi wote.
»
Previous
IGP Sirro kuwatumia Askari wastaafu Kibiti
Pages 22123456 »

No comments:

Leave a Reply