sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» » » Meneja wa tume ya uchaguzi aliyetoweka Kenya apatikana amefariki

Meneja wa tume ya uchaguzi aliyetoweka Kenya apatikana amefariki  

Meneja wa masuala ya teknolojia wa IEBC, alipatikana kwenye chumba kimoja cha kuhifadhi maiti mjini Nairobi
Image captionMeneja wa masuala ya teknolojia wa IEBC, alipatikana kwenye chumba cha kuhifadhi maiti cha City mjini Nairobi
Afisa wa cheo cha juu wa tume ya uchaguzi na mipaka nchini Kenya IEBC, ambaye alitoweka siku ya Ijumaa amepatikana akiwa amefariki.
Mwili wa Christopher Chege Musando, ambaye alikuwa kaimu mkurugenzi wa masuala ya teknolojia wa IEBC, umepatikana kwenye chumba kimoja cha kuhifadhi maiti jijini Nairobi
Mawasiliano ya mwisho kutoka mwa Musando aliyafanya siku ya Jumamosi mwendo wa saa tisa alifajiri kupitia ujumbe wa SMS kwa mmoja wa wafanyakazi wenzake.
Kisa hiki kinatokea ikiwa imesalia juma moja kabla ya kuandaliwa uchaguzi mkuu nchini Kenya ambao utafanyika tarehe 8 Agosti.
Polisi wanasema kuwa mwili wa afisa huyo pamoja na wa mwanamke ambaye hakutambuliwa, ilipatikana eneo la Kikuyu lililo vviungani mwa mji wa Nairobi na kupelekwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha City Mortuary.
Mkurugenzi mkuu wa IEBC Ezra Chiloba (kushoto) akiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha City
Image captionMkurugenzi mkuu wa IEBC Ezra Chiloba (kushoto) akiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha City
Bwana Musando alikuwa akihusika na usambazaji wa vifaa vya eletroniki ambavyo vingetumiwa kutambua wapiga kura na kwa upeperushaji wa matokeo wakati wa uchaguzi mkuu wiki ijayo.
Taarifa zinasema kuwa mwili wa Musando ulipelekwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha City Jumamosi asubuhi na watu waliojitambulisha kuwa maafisa wa polisi.
Tume ya IEBC, ambayo ilitangaza kutoweka kwake Jumapili, haijatoa taarifa yoyote rasmi kuhusiana na kupatikana kwa mwili wake.
Afisa mkuu mtendaji wa tume hiyo Ezra Chiloba hata hivyo amefika katika ufuo huo kutoa rambirambi kwa jamaa na marafiki wa marehemu waliofika kuuona mwili huo.
Mwili wa Bw Musando umesafirishwa hadi chumba cha kuhifadhia maiti cha Lee Funeral Home.
Mwili wa Musando ukiwekwa kwenye gari kupelekwa Lee Funeral Home
Image captionMwili wa Musando ukiwekwa kwenye gari kupelekwa Lee Funeral Home

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply