sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» » Uhuru Kenyatta atangazwa mshindi wa kura ya urais, Raila Odinga apinga

 Tume ya Uchaguzi nchini Kenya imemtangaza rais Uhuru Kenyatta kama mshindi wa Uchaguzi Mkuu wa urais uliofanyika siku ya Jumanne wiki hii.

Baada ya kuhakiki upya kwa fomu zinazoonesha matokeo zilizopewa jina la 34 A na 34 B kutoka maeneo bunge na vituo vya kupigia kura, Mwenyekiti wa Tume hiyo Wafula Chebukati amesema rais Kenyatta alipata kura Milioni 8.2  sawa na asilimia 54.2 dhidi ya mpinzani wake wa karibu Raila Odinga aliyepata kura Milioni 6.7 sawa na asilimia 44.7.
Ushindi huu unamaana kuwa rais Kenyatta alipata asilimia 50 na kura moja, ya jumla ya kura zilizopigwa lakini pia asilimia 25 ya kura zote angalau katika kaunti 24 kwa mujibu wa Katiba ya nchi hiyo.
Chebukati ameeeleza kuwa kati ya wapiga kura zaidi ya Milioni 19 waliojiadikisha kupiga kura, Wakenya takriban Milioni 15 walishiriiki katika Uchaguzi huo.
Ushindi wa Kenyatta umekataliwa na muungano wa upinzani NASA na kusema, kura za mgombea wake ziliibiwa na matokeo yalibadilishwa.
Kabla ya kutangazwa kwa mshindi, NASA walikutana na Makamishena wa IEBC na kueleza hoja zao ikiwa ni pamoja na kutaka wadau wote kuruhusiwa kuthathmini mfumo wa tume hiyo.
Hata hivyo, Mawakala wa Odinga ambao ni Musalia Mudavadi na James Orengo, wamesema madai yao hayajatatuliwa licha ya kuahidiwa na Tume hiyo mapema Ijumaa mchana.
“Pamoja na kwamba walikubali kushughulikia madai yetu, wamekataa kuyafanyia kazi, tunaodoka hapa Bomas,” amesema Mudavadi.
Katiba ya Kenya inaeleza kuwa, yeyote anayekataa matokeo anaweza kwenda Mahakamani lakini, NASA wameonesha kuwa huenda wasiende kulalamikia matokeo haya.
“Tunawaachia Wakenya waone kilichofanyika, imani yetu ipo kwa wakenya,” amesema Orengo.
Aidha, upinzani umewashtumu waangalizi wa Kimataifa na kusema kauli yao haikuwa sahihi kuhusu Uchaguzi huo.
“Mwangalizi wa Jumuiya ya Madola, rais wa zamani wa Ghana John Mahama, hana uhusiano mzuri na mgombea wetu kwa sababu ni mpinzani wa rais wa sasa Ghana ambaye ni mwandani wa mgombea wetu,” amesema Orengo.
"Hawa waangalizi walikimbilia uamuzi wa kusema kuwa Uchaguzi huu ulikuwa huru na haki, wangehakikiwa kwanza," ameongeza.
Kutangazwa kwa matokeo haya kumewahuzunisha wafuasi wa upinzani huku ikiwa ni furaha kwa wafuasi wa rais Kenyatta.
Hali ni ya wasiwasi katika ngome ya wafuasi wa upinzani hasa mjini Kisumu.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply