sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» »Unlabelled » FANYENI KAZI KWA MAHUSIANO NA SII MALUMBANO; MENEJA TRA MKOA WA SHINYANGA ERNEST MDEE

Kahama
Jan 22, 2014.

FANYENI KAZI KWA MAHUSIANO NA SII MALUMBANO; MENEJA TRA MKOA WA SHINYANGA ERNEST MDEE

WAFANYABIASHARA Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga wametakiwa kufanyakazi kwa maelewano na ushirikiano na Mamlaka ya Mapato (TRA) Wilayani hapa  kwa lengo la kukuza mahusiano mazuri baina ya Mlipa kodi na Mtoa kodi.

Hayo yalisemwa juzi na Meneja wa Mamlaka ya Mapato Mkoa wa Shinyanga Ernest Mdee katika kikao kilichojumuisha Wafanyabiashara kutoka katika sekta za Kilimo na Viwanda kilichofanyika mjini hapa.

Mdee alisema kuwa mfumo wa kulipa kodi ni rasilimali katika nchi tena zinazoendelea na kuongeza kuwa kama wanyabiashara wataweza kulipa kodi kwa muda muafaka kasi kungekuwa hakuna malumbano baina ya pande hizo mbili.

Alisema kuwa kama kuna mambo ambayo wafanyabiashara hawayaelewi katika mfumo mzima wa biashara zao basi Mamlaka yake ipo tayari kutoa mafunzo kwa ajili ya kuwawezesha kwa urahisi na unafuu zaidi ili waweze kufanya biashara zao vizuri.
Pia Meneja huyo aliwataka Wafanyabiashara kuwa na moyo wa ujaili katika kuwataja majirani zao wanaokwepa kulipa kodi huku wakidai kuwa mauzo yao ni madogo wakati mizigo wanayoshusha katika maduka yao ni mikubwa kuliko kabadirio ya awali..

Kuhusu malalamiko ya Wafanyabiashara kuhusu mashine mpya za kutoa risiti Meneja wa TRA Wilaya ya Kahama Peter Nkwabi  alisema kuwa mashine hizo nzuri na kuongeza kuwa kama kuna matatizo juu ya mashine hizo wafike katika ofisi husika ili waweze kupata maelekezo zaidi.

Nkwabi aliwataka Wafanyabiashara kuwa na ushirikiano katika mambo mbalimbali na Mamlaka yake na kuongea katika vikao vya pembeni halia mbayo haitakuwa msaada kwa wafanyabiashara hao.

”Jamani Wafanyabiashara wa Kahama kama  kuna matatizo baina ya maafisa wangu na nyinyi ni bora matatizo hayo tukayazungumza na kuyamaliza na sii kuyazungumza pembeni hali hii haita wasaidia”,Alisema Peter Nkwabi.

Awali kulikuwa na malalamiko baina ya Wafanyabiashara wa Kahama kuwa Maafisa wa TRA wamekuwa wakipita katika maduka yao kwa lengo la kufungua droo zao za fedha na kuwalazimisha kuhesabu fedha zao ilikuona mauzo yao kwa siku hali ambayo wawalikuwa wakiilalamikia.

Wafanyabiashara Wilayani Kahama wamekuwa wakikwepa kulipa kodi za serikali mara kwa mara hali ambayo maafisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania wakifika katika biashara za o wamekuwa wagumu katika kusema mauzo yao wanayouza kwa siku na hivyo kuwafanya Maafisa wa TRA kukaa katika maduka yao kwa siku nzima ili kuona na hivyo kuwafanya kuona kuwa wanaonewa.
                                         

 MENEJA WA MAMLAKA YA MAPATO MKOA WA SHINYANGA (TRA)ERNEST MDEE AKIONGEA NA WAFANYABIASHARA WA WILAYA YA KAHAMA JUU YA MATUMIZI YA MASHINE ZA( EFD)MJINI KAHAMA JANA
 MWENYEKITI WA TCCIA WILAYA YA KAHAMA MEJA MSTAAF MATALA  AKIWA NA MUANDISHI WA GAZETI LA HABARILEO MJINI KAHAMA RAYMOND MIHAYO KABLA YA KIKAO CHA WAFANYABIASHARA NA MAMLAKA YA MAPATO MKOA WA SHINYANGA NA KAHAMA JUU YA MASHINE ZA (EFD )JANA MJINI HAPA
 BAADHI YA WAFANYABIASHARA WA MJI WA KAHAMA KABLA KUANZA KIKAO KATIKA UKUMBI WA NITESHI JUU YA MASUALA HULIPAJI WA KODI NA MASHINE ZA( EFD)
 MENEJA WA TRA MKOA WA SHINYANGA ERNEST MDEE AKITOA MAELEZO  KWA WAFANYABIASHARA JUU YA ULIPAJI WA KODI YA MAPATO  WILAYANI KAHAMA JANA
 MENEJA WA MAMLAKA YA MAPATO MKOA WA SHINYANGA AKIONYESHA WAFANYABIASHARA MASHINE YA( EFD) JINSI ILIVYO JANA KATIKA UKUMBI WA NITESHE JUU YA MATUMIZI ZA MASHINE HIZO
WAFANYABIASHARA WA WILAYA KAHAMA MAHOLELO MASUKA, WAKIMSIKILIZA KWA MAKINI  MENEJA WA MAMLAKA YA MAPATO MKOA WA SHINYANGA  ERNEST MDEE ,JANA KATIKA KIKAO CHA KUFAHAMISHANA JUU YA MASHINE ZA( EFD)

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply