sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» »Unlabelled »

 MKUU WA MKOA WA SHINYANGA ALLY RUFUNGA AKIDHIDUA MRADI WA MAJI KATIKA MADHIMISHO YA MAJI KIMKOA YALIFANYIKA KATIKA KIJIJI CHA KAGONGWA WILAYANI KAHAMA


Kahama
March 26, 2014.

WANANCHI WATAKIWA KUDUMISHA AMANI

WATANZANIA wametakiwa kudumisha amani hapa Nchini  ili waweze kufaidika na Matunda ya Serikali ya Chama cha Mapinduzi ( CCM) katika utekelezaji wa Ilani yake kwa Wananchi hasa katika sekta ya Maji kwa ujumla.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga Khamis Mgeja aliyasema hayo katika sherehe za kilele cha wiki ya maji iliyofanyika kimkoa katika Kijiji cha Kagongwa WilayanI Kahama huku akisisitiza kuwa Chama cha mapinduzi kipo pamoja na Wananchi wake katika kutekeleza ilani yake hasa katika sekta ya maji.

Mgeja alisema kuwa Sekta ya maji ni moja kati sera ya Chama cha Mapinduzi na kuongeza kuwa Chama hicho kitaendelea kuisimamia Serikali katika kuhakikisha kuwa sera za Chama hicho zinatekelezwa ipasavyo kwa Wananchi ikiwemo ile ya maji hasa katika maeneo ambayo huduma hiyo imekuwa haipatikani.

“Chama cha Mapinduzi ndio jawabu ya majibu ya matatizo ya Watanzania na sii kukimbilia chama kingine ambapo ni sawa na kutokuwa na mwelekeo na majawabu ya majibu yenu hayawezi kupatikana”, Alisema Khamis Mgeja Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga.

Mwenyekiti huyo wa CCM Mkoa wa Shinyanga aliendelea kusema  kuwa kwa sasa malumbano kati ya Wana CCM Mkoa wa Shinyanga kwa sasa hayana tija na badala yake wanachama wa  chama hicho waungane ili kuweza kukiimarisha Chama hicho hali ambayo itaondoa migongano ndani ya chama hicho.

Aliendelea kusema kuwataka Wana CCM Mkoa wa Shinyanga  kuzungumzia maendeleo kwa sasa kwani  Mkoa huo unajivunia kuwa Viwanda pamoja na Rasilimali nyingi na kuongeza kuwa wanachama cha Mapinduzi wasisite kuzungumzia maendeleo kwa kipindi hiki cha sasa.

Hata hivyo Mgeja aliwataka wananchi wa Mkoa wa Shinyanga kuwa na imani na Chama cha Mapinduzi kwani kimewatoa mbali tangu uhuru na ndio chama pekee inachoweza kutatua matatizo ya Watanzania pamoja na kero za mbalimabali walizo nazo.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Ally Rufunga aliyekuwa Mgeni Rasmi katika sherehe alisema kuwa kwa mwaka huu Serikali Mkoani Shinyanga imejitahidi kuondo kero za maji kwa Wananchi wake lakini baadhi ya Wananchi wamekuwa wazito katika kuchangia gharama za maji katika maeneo yao wanayoishi.

Rufunga alisema kuwa kuna baadhi ya maeneo Serikali imekwishatoa fedha kwa ajili ya miradi ya maji lakini Wananchi wamekuwa wazito katika kuchangia gharama kidogo zinazotakiwa kutolewa kwa ajili ya kukamilisha miradi hiyo.

mwisho

MWENYEKITI WA CCM MKOA WA SHINYANGA KHAMIS MGEJA AKITWISHA NDOO YA MAJI MJUMBE WA KAMATI YA MAJI REGINA NYANDA KATIKA KIJIJI CHA KAGONGWA AMBAPO KIMKOA ILIFANYIKA WILAYANI KAHAMA PICHA NA MOHAB DOMINICK

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply