sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» »Unlabelled » WATANZANIA WATAKIWA KUTOACHAGUA KAZI ZA KUFANYA



                                                                                                                                                                             
Na  Mohab Dominick
Kahama
Mrch 30, 2014.

WATANZANIA WATAKIWA KUTOACHAGUA KAZI ZA KUFANYA

WATANZANIA wakubwa   na Vijana wameshauriwa wasichague kazi za kufanya badala yake wafanye kazi halali za kuwaingizia kipato na maslahi yao  halali kuliko ya kufanya zile ambazo zipo juu ya uwezo wao usiokuwa halali ambapo kwa sasa imekuwa kama ugonjwa mwingine unaolitafuna taifa .

Hayo yalisemwa juzi na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga Khamis Mgeja wakati alipokuwa akikabidhi Msaada wa Luninga yenye tahamani ya shilingi 260,000 kwenye kijiwe maarufu cha wajasiliamali cha  Kahawa maarufu kwa jina la BBC katika mji mdogo wa Isaka Wilayani Kahama.

Mgeja alitoa Msaada huo kutokana na ambi aliloombwa na Wajasilimali wa kundi la BBC  alipofanya ziara ya kikazi ya chama ya kukagua shughuli za utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi  mwaka katika Mji huo mdogo wa Isaka.

Wajasiliamali hao waliomba msaada huo wa Luninga ili waweze kupata habari kupitia chombo hicho hasa nyakati za asubuhi na jioni kabla ya kazi na baada ya kazi ili kwenda sambamba na mambo yanatokea ndani na nje ya nchi.

Akipokea msaada huo wa Luninga kutoka kwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga Khamis Mgeja, Mwenyekiti wa Wajasilimali hao wa BBC Ali Salumu Msangi alishukuru na kuongeza kuwa msaada huo umefika katika kipindi muafaka hasa wakati wa kipindi hiki cha Bunge la katiba linaloendelea Mjini Dodoma.

Baada ya makabidhiano ya zawadi hiyo Mgeja aliwataka wazee na vijana wajenge utamaduni wa kuridhika vipato vidogo wanavyovipata kulingana na hali waliokuwa nayo badala ya kukimbilia vipato vya juu ambavyo vipo nje ya uwezo wao wa kimataji.


Mgeja pia alisema kuwa  hapa nchini bado kuna fursa mbalimbali ambazo zinaweza kuwakwamua kiuchumi watanzania hususani Vijana na  wale wa kawaida hasa katika sekta za Kilimo, Uvuvi, ufugaji pamoja na uanzishwaji wa  Viwanda vidogovidogo.

“Hapa nchini bado kuna fursa nyingi  mbalimbali za kuinua uchumi kwa wananchi wa kawaida hasa katika sekta za Kilimo, uvuvi, na hata ufugaji hali ambayo inaweza kuleta mabadiliko kwa vijana wenye kipato kidogo”, Alisema Mwenyekiti huyo wa Mkoa wa Shinyanga.

 Mwisho






«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply