Kahama
April 13,
2014.
MASHINDANO YA MPESYA CUP YAANZA KUTIMUA VUMBI
KAHAMA.
SERIKALI Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga imesema
kuwa haitawatupa Vijana hasa katika masuala mazima ya michezo kwa lengo la
kuinua uchumi wa Wilayani hii sambamba na kupata timu itakayoshiriki ligi kuu
kwa miaka ya mbele.
Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mpesya aliyasema hayo
wakati akifungua mashindani ya Mpira wa miguu maarufu kama Mpesya cup ambayo
yanashirikisha jumla ya timu 26 za Wilaya ya Kahama.
Mpesya alisema kuwa haiwezekani Wilaya ya Kahama
pamoja na kuwa rasilimali nyingi ikiwemo wawekezaji katika sekta za migodi na
Tumbaku wapo lakini Wilayah ii inakosa timu inayishiriki ligi kuu hapa nchini.
Aidha alisema kuwa lengo la mashindano ya Mpesya cup
ni kukuza vipaji kwa Vijana wa Wilaya ya Kahama sambamba na kutafuta wachezaji
ambao wataunda timu ya kombaini ya Wilaya ya Kahama ambayo itashiriki katika
mashindano mbalimbali.
Mkuu huyo wa Wilaya ya Kahama aliendelea kusema kuwa
mpira ni starehe na inakuza akili na kungeza kuwa kwa sasa pia ni ajira hali
ambayo itawafanya wachezaji kufanya michezo kama sehemu yao ya kujipatia
kipato.
“ Kwa sasa tumedharia Wilaya ya Kahama lazima tupate
timu itakayocheza ligi kuu kwa hali tunayo na Rasilimali tunazo na wachezaji
tumieni michezo katika katika kuonyesha viapaji vipaji vyenu ulionavyo”,
Alisema Mkuu wa Wilaya ya kahama Benson Mpesya.
Pia aliwataka wachezaji kutumia michezo kama sehemu
ya kujenga urafiki na mahusiano mazuri
na kutoa onyo kwa waamuzi mashindano hayo kuhakikisha kuwa wanachezesha michezo
hiyo kwa kufuata sheria 17 za soka.
Katika michezo hiyo hiyo ya Mpesya cup mshindi wa
kwanza atapata zawadi ya shilingi milioni moja pamoja na seti moja ya jezi,
kikombe na mpira mmoja wakati wa pili
atapa kiasi cha shilingi 500,000 pamoja na seti moja ya jezi na mpira .
Michuano hiyo tayari imeanza juzi kwa mechi moja
katika timu ya Ngaya FC na Ambassador na kumalizika kwa matokeo ya timu ya
Ambassador kuinfunga timu ya Ngaya FC kwa jumla ya mabao 2-1.
Matukio katika picha
Mwenyekiti wa ccm mkoa wa shinyanga khamis mgeja mwenye jackty jeupe kushoto kati ni mkuu wa wilaya ya kahama Benson mpesya wakiwa katika mandamano ya ufungunzi wa mpesya cup
Baadhi ya wanamichenzo wakiwa na mabango ya kuonyesha michenzo ni ajira michenzo amani
mmoja wa shambiki wa timu ya Nganya akiwa na furaha ya siku ya uzinduzi wa kombe la mpesya cup
Baadhi ya timu mbali mbali ambazo zitashiriki mpesya cup mjini kahama
Mmoja mama shabiki lilopo juu ya pikipiki likifurahi uzinduzi wa kombe la mpesya cup
No comments: