sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» »Unlabelled » WANANCHI KAHAMA WASIKITISHWA NA WAJUMBE WA BUNGE LA RASIMU MPYA KUTOELWANA.



Na  Mohab Dominick
Kahama
April 23, 2014.


WANANCHI Wilayani Kahama  Mkoani shinyanga wamesikitishwa na vitendo vinavyofanywa na Wajumbe  wanaojadili Rasimu mpya ya Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kitendo cha kutoelewana katika majadiliano yao hali ambayo inafanya wakati mwingine baadhi ya Wajumbe kutoka nje ya ukumbi wa Bunge.

Wakitoa maoni yao na gazeti la nipashe  Wananchi hao walisema kuwa kitendo cha wajumbe wa Bunge hilo la rasimu ya  katiba mpya  kutoelewana kila siku kunasababisha hadi wananchi kutokuwa na hamu ya kuliangalia kwa kuwa wanakuwa na wasiwasi kama katiba ya nchi hii itapatikana kwa staili hiyo.

Wanasema kuwa kwa sasa wakati wananchi wa nchi nzima macho yao yakiwa katika mji wa Dodoma kusikiliza Bunge hilo ni bora wakakaa kwa utumilivu na kujadili rasimu hiyo bila ya kuwa na malumbano yeyote kwani kwa zimebaki siku chache tuu za kujadili Rasimu hiyo lakini mpaka kuifikia hivi sasa bado watanzania bado hawajapata jibu kuhusu majadiliano ya bunge hilo.

“Kwa sasa Wananchi wamekuwa hawana imani na Bunge hilo linaloendelea Mjini Dodoma hali ambayo imefanya wengi wao hata kukata tama ya kuliangalia kwani wanasema kuwa bunge hilo kwa sasa limekuwa tofauti na watanzania walivyokuwa wakidhani litakuwa kwa manufaa yao”,Walisema Wanachi hao.

Mmoja wa wananchi hao ambaye ni Diwani wa Kata ya Bugarama Nickson Igoko alisema kuwa kwa sasa Wajumbe hao wa Rasimu ya Katiba Mpya kukaa na kuelewana kwani jicho la Watanzania linawaangalia wao kwa sasa ili kuweza kupata mustakabali wan chi yao kwa miaka 50 ijayo.

“Tukishindwa kujadili Rasimu hii ni kama kupoteza Mwelekeo wa Watanzania hasa wengi wao wakiwa maeneo ya Vijijini ambapo hawajui chochote kinachoendelea hadi sasa hali ambayo itakuwa ni kama kutowatendea haki watu hao”, Anaongeza Nicksoni Igoko Diwani wa Kata ya Bugarama (CCM)

Alisema kuwa wakati wajumbe wa rasimu hiyo wakichaguliwa watanzania wengi walikuwa na imani nao hali ambayo kwa sasa imekuwa tofauti kwani kila siku kumekuwa na malumbano baina ya watu pande mbili hali ambayo kwa sasa zimebaki siku 12 kusitishwa kwa bunge hilo bila ya kuwa hata na mwelekeo hata mmoja kwa kupatikana kwa Katiba hiyo.

Igoko aliendelea kusema kuwa kusitishwa kwa Bunge hilo bila ya kuwa na mwelekeo kwa kipindi cha miezi mitatu waliokaa ni kama kuwatania watanzania ukizingatia kodi za Wananchi zinapotea kwa wajumbe hao kulipwa posho kwa kipindi hicho hali ambayo inafanya wananchi kuwapotezea hamu ya  kuliangalia bunge hilo.

“Ni bora bunge hilo lingekuwa na watu 30 tuu ambao wangekaa kwa kuelewana hali ambayo hadi kufikia hivi sasa wananchi wangekuwa tayari wamepata picha ya katiba yao ingekuwa vipi kuliko kukalia kubishana bila ya kuwa na mafanikio yeyote na kuwajengea watanzania hofu ya kupatikana kwa katiba hiyo mpya”, Alisema Diwani huyo

mwisho

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply