sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» »Unlabelled » MADIWANI MJI KAHAMA WAMKATAA MGANGA MKUU WA HOSPITALI YA WILAYA



  MADIWANI MJI KAHAMA WAMKATAA MGANGA MKUU WA HOSPITALI YA WILAYA


Na  Mohab Dominic
Kahama
May 22, 2014.

BARAZA la Madiwani la Halmashauri ya Mji wa Kahama juzi lilimkataa Mganga Mkuu wa Hospitali ya Halmashauri hiyo Helen Membe kwa kile walichesema kuwa hana sifa za kuongoza Madaktari wenye sifa na watumishi wanaohudumia Wagonjwa katika Hospitali hiyo
.
Diwani wa Kata ya Majengo Bobson Wambura alisema kuwa Mganga Mkuu huyo amepewa wadhifa huo huku akiwa hana sifa hata moja ya kuwa na cheo hicho hali ambayo imefanya kuwepo na makundi ya Wafanyakazi wa Hospitali hiyo pamoja na Waganga.

Alisema kuwa kutokana na Dr, Huyo Helen Membe kutokuwa na sifa za kuongoza watumishi wa Hospitali hiyo pia kumesababisha kuwepo kwa migomo baridi ya Madaktari hali ambayo imefanya Wagonjwa kutopata huduma kwa wakati muafaka.

Kwa sasa Mheshimiwa Mwenyekiti kumekuwa na makundi makubwa  katika Hospitali hiyo kuanzia Madaktari, Wauguzi na Wafanyakazi wengine huku wakisema ni vigezo gani vimepelekea Daktari huyo kupata wadhifa huo mkubwa”, Alihoji Bobson Wambura Diwani wa Kata ya Majengo.

Aliendelea kusema kuwa kuhusu Mganga Mkuu huyo ni bora Wizara ikiwa wazi juu ya Mtumishi huyo kwani ni mzigo na hana uwezo kuliko wale waliopo chini yake hali ambayo imezua migogoro mingi isiyoisha katika Hospitali hiyo baina ya Wafanyakazi na kiongozi huyo.

Diwani huyo aliendelea kusema katika Baraza hilo kuwa kwa sasa katika Hospitali ya Wilaya baadhi ya Madaktari wamekuwa wakifanya kazi katika Hospitali binafsi za watu huku wakiwaacha wagonjwa wakipata taabu ya kutafuta huduma ya tiba katika Hospitali hiyo ya Wilaya.

“Ukienda sasa Hivi katika Hospitali ya Wilaya kutafuta huduma huwezi kupata kwani madaktari wanafanya kazi katika Hospitali za Watu binafsi na Wagonjwa wanabaki bila ya kuhudumiwa na inashangaza sana tunaomba kiongozi huyo abadilishwe kwani kuna watu wenye sifa ya kuwa cheo hicho kuliko daktari huyo”, Alisema Diwani huyo. 

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Kahama Felix  Kimaryo akijibu hoja hiyo aloisema kuwa suala hilo limeishafika katika Ofisi yake na linashughulikiwa ipasavyo ili kuhakkikisha wananchi kero inaondoka haraka iwezekanavyo katika Hospitali hiyo ya Wilaya.

“Ndugu zangu Madiwani subirini masuala yanayohusu Hospitali ya Wilaya yanashughulikiwa kwa mujibu wa kufuata sheria na taratibu na sii lazima kusema hatua zinazochukuliwa na Halmashauri juu ya Mtumishi huyo mbele Baraza zima la Madiwani kwani kikao hiki ni cha wazi”, Alisema Felix Kimaryo Mkurugenzi wa Halmashuri ya Mji.

mwisho

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply