sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» »Unlabelled » 2508 WAJIUNGA KIDATO CHA KWANZA MWAKA JANA KAHAMA



Na Mohab Dominick
Kahama
May 23, 2014.

2508 WAJIUNGA KIDATO CHA KWANZA MWAKA JANA KAHAMA

JUMLA ya Wanafunzi wapatao 2508 waliomaliza darasa la saba mwaka jana wamejiunga na kidato cha kwa kwanza katika shule mbalimbali za binafsi na za Serikali Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga ikiwa ni sawa na asilimia 86 ya Wanafunzi wote waliofanya mtihani.

Hayo yalisemwa juzi na Afisa Elimu Sekondari wa Halmashauri ya Mji wa Kahama Anastazia Manumbu katika baraza la Madiwani la Halmashauri hiyo lililofanyika juzi Mjini Kahama na kuongeza kiwango kilichokuwa kimepngiwa kwa ni Wanafunzi 2931.

Manumbu aliesema kuwa katika idadi hiyo ya Wanafunzi waliofaulu mtihani wa kumaliza darasa la saba kwa mwaka jana 2013 wanawake 1331 huku wale wakiume wakiwa idadi ya Wanafunzi 1600.

Afisa Elimu huyo aliendelea kusema kuwa jumla ya Wanafunzi 547 walijiunga katika shule za sekondari na Binafsi wakati idadi ya Wanafunzi 1963 walijiunga katika Shule za sekondari za Serikali na hivyo kutimia idadi hiyo ya Wanfunzi 2508.

Akielezea kwa upande wa shule za shule za Sekondari Afisa Elimu huyo Manumbu alisema kuwa kiwango cha ufaulu kwa Wanafunzi wa kidato cha nne kwa mwaka jana kimeongezeka kwa asilimia 74 ukilinganisha na miaka ya nyuma.

Akizungumzia kuhusu mikakati ya Mkoa ya Mkoa wa Shinyanga kwa Wilaya ya Kahama katika kukuza Elimu ya Sekondari Manumbu aliesema kuwa mkoa umejipanga kwa kuweka mitihani ya utimilifu pamoja na ile ya pamoja pamoja na mitihani ya mwisho.

Hata hivyo aliendelea kusema kuwa gharama za mitihani hiyo itanchangiwa na Wazazi wa Wanafunzi huku kiwango cha mitihani hiyo kikiwa jumla ya shilingi 10,000 kwa kila mwanafunzi atakayewajibika kufanya mitihani hiyo,

mwisho

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply