Na Mohab
Dominick
Kahama
May 6, 2014.
MGEJA; KAULI YA LEMBELI CCM SIO MAMA YAKE NI
KUVIMBIWA MADARAKA
CHAMA cha Mapinduzi Mkoa wa Shinyanga kimesema kuwa
kauli ya Mbuge wa Jimbo la Kahama James Lembeli ya kusema kuwa Chama cha
Mapinduzi (CCM) sio mama yake ni kama kitendo cha kuvimbiwa Madaraka aliyokuwa
nayo.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga Khamis Mgeja
alitoa kauli hiyo wakati akiwahutubia wakazi wa Kata Isaka katika ziara yake ya
kuzungumzia maendeleo amani na Upendo na katika Wilaya ya Kahama pamoja na
kukagua shuguli za maendeleo kama ilani ya chama hicho inavyosema.
Mgeja alisema kuwa wao kama chama cha mapinduzi Mkoa
wa Shinyanga wamekuwa wakipokea simu mbalimbali kutoka kwa wadau kulaani
kitendo hicho kilichosemwa na Mbunge huyo tena mbele ya vyombo vya habari.
Aidha Mwenyekiti huyo alisema kuwa Chama cha
Mapinduzi ndicho kimemfikisha Mbunge huyo hadi alipo na kimemfanya hadi kupata
fursa za kutembelea hadi nchi za nje lakini kwa kauli yakje hiyo aliyoisema
inakuwa aileti tija kwa chama hicho ambacho hadi hivi sasa ni Mbunge kupitia
CCM.
“Sisi hatuna taabu juu ya mambo mengine yanaymhusu
yeye kama kuunga mkono Serikali tatu lakini sisi kama Wananchama wa Chama cha
Mapinduzi Mkoa wa Shinyanga tunapingana na kauli yake moja tu ya kusema Chama
cha Mapinduzi sio mama yake”,Alisema Khamis Mgeja Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa
Shinyanga.
“Leo katika Mkano huu sina nafasi ya kuzungumzia
kuhusu kauli ya Mbunge huyu kwani Katibu wa Itikadi na uenezi wa Mkoa
alishayasema haya hapo awali na kutuwakilisha uongozi wa Mkoa wa Shinyanga
katika kulaanui kitendo cha Mbunge huyo
tena wa CCM”, Aliongeza Khamis Mgeja.
Pamoja na Mambo mengine katika Mkutano huo Mgeja
aliwataka watanzania kuungano juu Serikali mbili katika mchakato wa kupata
katiba mpya mpya na kuwataka viongozi wa matawi ya CCM kuwaambia wananchi wao
juu faida za Serikali mbili badala ya kushabikia Serikali tatu kama walivyo
wabunge wa upinzani.
Pia Mwenyekiti huyo wa CCM Mkoa wa Shinyanga alisema
kuwa kitendo cha viongozi kupenda Serikali tatu ni kama mkitendo cha
kuwabebesha watanzani mzigo na kuongeza kuwa Serikali tatu ipo pamoja na
ukiunganisha Seriali za Mitaa lakini bado watanzania hawajajua hivyo.
Mwisho.
No comments: