sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» »Unlabelled » WAANDISHI WA HABARI NI LULU YA WANYONGE



WAANDISHI WA HABARI NI LULU YA WANYONGE

Na Mohab Dominick
Shinyanga

Imeelezwa kuwa waandishi wa habari hapa nchini ni mkombozi wa wanyonge hasa pale wanapoandika habari za kijamii na kufichua maouvu yanayofanywa na baadhi ya viongozi walioko kwenye madaraka kwa kushindwa kutekeleza miradi ya maendeleo pamoja na kuzitafuna fedha hizo

Hayo yamezungumzwa jana na meneja wa CRDB tawi la shinyanga mjini Saidi Pamuye wakati akisoma hotuba katika siku ya uhuru wa habari kwa wanahabari wa mkoani shinyanga katika maadhimisho hayo

Pamuye alisema asilimia kubwa ya jamii hasa wale waishio maeneo ya vijijini wamekuwa hawapati huduma zao muhimu pamoja na kutendewa matendo maovu na baadhi ya watu wenye kipato wakiwemo na viongozi wa serikali ambao wamekuwa wakila fedha za miradi zinazotolewa kuwatekelezea miradi yao

Alisema chombo pekee chenye kuwasemea wanyonge hao kwa serikali na kuwasaidia kupata haki zao kwa baadhi ya watu wachache wanaohujumu miradi yao na kuwakandamiza, ni vyombo vya habari ambavyo ndivyo vyenye sauti kubwa ya kufikisha ujumbe wao kwa walengwa na kuweza kutatulliwa matatizo yao

Akizungumza katika maadhimisho hayo mkuu wa upelelezi mkoani shinyanga Hussein Kashidye aliwataka wanahabari wa mkoa huo licha ya kukabiliana na changamoto wanazokumbana nazo bali wafanye kazi kwa ufanisi na weledi kwa kuzingatia sheria za uandishi na kufichua maovu bila ya kuwa na uoga

Kashidye alisema wanahabari ndio nguzo pekee iliyobaki ya kufichua maouvu na kuyakemea na kuifanya jamii iweze kuishi kwa amani na upendo hivyo wanawajibu wa kutafuta habari za uchunguzi huku wakishirikiana na Jeshi la polisi kwa kupeana taarifa mbalimbali ambazo zitasaidia kuondoa changamoto hizo kwa wananchi

“wanahabari ndio nguzo pekee iliyobaki ya kufichua maovu yanayofanyika ndani ya jamii pamoja na serikali kwa kutoa taarifa kwa kupitia vyombo,na sisi kama Jeshi la polisi tukipata habari hizo tunazifanyia kazi na pia tunaomba tushirikiane  natufanye kazi kwa pamoja kukemea matendo hayo maovu”alisema Kashidye

Aliongeza ‘licha ya kuandika habari za maovu yanayofanywa na baadhi ya viongozi wa serikali pia jeshi tunaomba muandike habari za kukemea mauaji ya vikongwe na Alibino ambayo bado yanaendelea katika mkoa wetu kutokana na imani za kishirikina,Mila potofu pamoja na kugombania Mirathi”

Naye Afisa vipimo wa mkoa wa Shinyanga Juma Chacha aliwataka wanahabari wa mkoa huo kuacha kutumiwa na baadhi ya wadau kwa kuandika habari zenye manufaa yake binafsi kwa kupewa fedha na kuacha kuandika ukweli hali ambayo itaendelea kuwa didimiza wanyonge na kurudisha maendeleo ya kiuchumi kwa jamii

“Sasa wanahabari umefika wakati wa kutoa taarifa kwa uhuru  bila ya kujali wadhifa wa mtu wala cheo chake kwa kuandika habari zenye kufichua maouvu, mfano sisi wakala wa vipimo kipindi cha msimu wa zao la pamba tumekuwa tukipata wakati mgumu pale tunapofanya kazi yetu ya kukagua vipimo na kukukata vipimo hivyo vimechezewa na kumuibia mkulima” alisema Chacha

“Na pale tunapowakamata wahusika na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria lakini asilimia kubwa tumekuwa hatusikii habari zao zikitolewa kwenye vyombo vya habari hali ambayo inatupa wasisi wasi kuwa labda mmepewa kitu kidogo ilimsitoe habari”mwisho







«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply