Na
Mohab Dominick
Kahama
May
6, 2014.
MWALIMU
AUWA MWANAFUNZI KAHAMA
MWANAFUNZI mmoja mkazi wa wa Jijini Mwanza Clinton
Majembe ameuwawa kwa kupigwa na mama yake wa kambo Lupinda Kauli Mwalimu wa
Shule ya Msingi Malunga mjini Kahama kwa kinachodaiwa kuwa kuwa mtoto huyo
aliacha jiko jiko la gesi likiwa linawaka ndani.
Kwa
mujibu wa Mwenyekiti wa Mtaa wa Majengo Noel Mseven ambapo tukio hilo lilitokea
usiku wa kuakia Ijumaa kuu alisema kuwa Marehemu alikuwa ni Mwanafunzi wa
kidato cha pili katika shule moja mjini Bukoba.
Mseveni
alisema kuwa Marehemu Clinton alikuja kumsalimia mama yake wakati wa likizo
ndogo ya pasaka na hivyo kumkosa hali ambayo ilisababisha mama yake huyo wa
kambo aliyekuwepo katika nyumba hiyo kupiga kutokana na kudai kuwa alikuwa
amewasha jiko la gesi bila ya idhini yake.
Alisema
kuwa Mama huyoa ambaye ni mtu wa matukio katika mtaa huo pia inasadikiwa pia
aliwahi kmtishia mume wake kumuua na hivyo kusababisha kuukimbia mji wake mpaka
kufikia hivi sasa.
Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Shinyanga Ernest Mangala amethibitisha kutokea kwa tukio hilo
na kudai kuwa kwa sasa hayupo ofisi yupo nje kikazi na kuhaidi kulizunguzia
tukio hilo pindi atakaporejea kazini hivi karibuni.
Mwisho.
No comments: