headlines

sponsor

sponsor

Slider

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» » POLISI WACHANA BANGO LA WALIMU LINALOHOJI POSHO LA BUNGE MAALUMU LA KATIBA.
 Mohab Dominic



 mabango ya walimu yanayohusu mapujo ya mishahara yao



Bukoba. 

 Maandamano ya walimu kuingia katika Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba kuadhimisha Siku ya Walimu Duniani, jana yalipata mtafaruku baada ya polisi kuyaingilia na kuchana bango mojawapo lililohoji posho za wajumbe wa Bunge la Katiba.

Bango hilo la kitambaa cheupe lilikuwa na maandishi yanayohoji posho ya Sh300,000 waliyokuwa wanapata wajumbe wa Bunge la Katiba, yakilinganishwa na kazi kubwa wanayofanya walimu.

Ujumbe wenyewe ulisomeka hivi: “Haki iko wapi usawa uko wapi, posho ya mjumbe wa Bunge la Katiba kwa siku shilingi laki tatu, mshahara wa mwalimu shilingi 370 kwa mwezi. No big results without big salary (Hakuna matokeo makubwa bila mshahara mkubwa)”.

Ujumbe huo ulikuwa ukifanya rejea ya viwango vya malipo ya Sh300,000 kwa siku ambazo walikuwa wakilipwa wajumbe wa Bunge Maalumu zikiwa ni Sh230,000 kama posho ya kujikimu na Sh70,000 ambazo ni posho ya vikao.
Hata hivyo bango hilo lilichanwa hatua chache kabla ya walimu hao hawajaingia uwanjani humo, ambapo mgeni rasmi alikuwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.

Mwenyekiti wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), mkoani Kagera Dauda Bilikesi, alisema amesikia habari za bango hilo kuharibiwa lakini akasema asingezungumza kwa kina kuhusu suala hilo kwa kuwa hayo yamepita.

Waibuka na shairi.

Muda mfupi baada ya polisi kuharibu bango hilo lisionekane uwanjani, walimu hao walipiga chenga kiana wakaibuka na ujumbe ule ule kwa njia ya shairi.
Kupitia shairi hilo liliposomwa mbele ya Pinda, walimu walihoji ukubwa wa posho za wajumbe wa Bunge la Katiba zikilinganishwa na mshahara wanaopata, hali iliyosababisha umati wa walimu uliokuwa uwanjani hapo kulipuka kwa sauti kubwa za shangwe.

Shairi hilo lililosomwa na Mwalimu Betwel Magoso kutoka Wilaya ya Biharamulo, lilisababisha kuvurugika kwa muda kwa utaratibu uliopangwa kwa mujibu wa ratiba, pale alipohoji wajumbe wa Bunge la Katiba kupata Sh1 milioni kwa siku tatu ambazo ni mkopo wa mwalimu kwa miaka mitatu.

Mwalimu Magoso alimgusa Pinda ambaye kabla ya kuanza hotuba yake alianza kwa kusema kuwa mwalimu huyo alitumia ujanja kufikisha ujumbe wake na kuwa baadhi ya maneno katika shairi lake yalikuwa ni mazito. 

Mwisho.

 


«
Next
ALIYEMLAWITI MTOTO WA DARASA LA TATU AACHIWA HURU NA ASKARI POLISI JIJINI DAR.
»
Previous
LEMBELI:CCM ILINIHUJUMU UCHAGUZI 2010!!! ASEMA ILITENGENEZA JIMBO BANDIA LA USHETU ILI ASIPATE UBUNGE.!!
Pages 22123456 »

No comments:

Leave a Reply