sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» » SERIKALI ZA VIJIJI ZIKAGUE PAMBA KABLA YA KUUZWA



 SERIKALI ZA VIJIJI ZIKAGUE PAMBA KABLA YA KUUZWA

WADAU pamoja na Wanunuzi wa zao la Pamba Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga wameziomba Serikali za Vijiji  katika msimu ujao wa ununuzi wa zao hilo kukagua Pamba kabla ya kufikishwa sokoni ili kuepusha kuwepo kwa pamba chafu na zinazowekewa maji na Michanga.

 Meneja Kampuni ya ununuzi wa zao la Pamba ya KCCL Wilayani Kahama Bahati Mayala alisema kuwa kwa kushirikishwa viongozi wa Serikali za vijiji katika kukagua Pamba kabla ya kufikishwa sokoni kunaweza kusaidia pamba ya tanzana kurudi katika soko la kimataifa kama ilivyokuwa zamani.

Malaya alisema kuwa kwa sasa Changamoto kubwa inayowakabili wanunuzi wa zao hilo ni pamoja wakulima wengi kuweka maji pamoja na mchanga ili kuongeza uzito wakati Pamba inapokuwa sokoni hali inafanya zao hilo kushuka ubora wake katika soko la Dunia.

Alisema kuwa kwa kushirikiana na uongozi wa serikali za Vijiji katika kukagua Pamba kama ilivyokuwa miaka ya nyuma inaweza kuwa suluhisho sahihi na kupunguza uchafy katika zao la Pamba ambalo kwa sasa linaonekana kupteza mwelekeo hasa katika kanda ya ziwa ambapondipo lilikuwa likilimwa kiasi kikubwa.

Mayala alizitaja baadhi ya Wilaya ambazo ndizo zimekuwa kinara wa kuchafua Pamba kuwa ni pamoja na Kishapu, Meatu, Igunga pamoja na Maswa na kuongeza kuwa Wilaya ya nzega ndio pekee ambayo imekuwa kitoa Pamba safi tofauti na nyingine.

Pia Meneja huyo aliitaka Serikali kutunga sheria ya kutaka pindi Mkulima anapobainika kuchafua Pamba kwa makusudi achukuliwe hatua kali za kisheria kwa kuwatumia wataalu wake yaani maafisa ugani waliopo katika maeneo husika hali ambayo itakuwa ni chachu kwa wakulima kuuza Pamba iliyo safi.

Akizungumzia kuhusu kilimo cha Mkataba Meneja huyo wa Kampuni ya KCCL alisema kuwa kilimo hicho kimeku kigumu kutokana na baadhi ya Wakulima kukwepa kulipa madeni hali ambayo inakuwa ikitia hasara Makampuni ya ununuzi wa zao huilo la Pamba.

Aidha alisema kuwa katika Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita wanadai jumla ya madeni ya shilingi milioni 80 zinzotokana na mikopo ya Pembejeo, Mbegu pamoja na dawa na hivyo kuisababishia Kampuni hiyo hasara kubwa huku Kampuni hiyo ikisambaza mbegu tani 15,000 katika msimu uliopita.
mwisho


«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply