sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» » SHINYANGA YAPIGA MARUFUKU BIASHARA YA NGONO

 Baadhi ya kinadada wanafanya biashara za ngono.
 Mmoja wa dada poa akiwa katika ofisi yake kusubiri wateja wake.
 Tupo kazini ndiyo maneno ya kinadada poa wakiwa nje ya uwanja wa maduka mengi mjini shinyanga .
 Best hali ni mbaya hayo ndiyo maneno yakinadada hawa wakitafakali juu ya  maisha kuwa ngumu baada ya mkuu wa mkoa wa shinyanga kupinga marufuku biashara hiyo ya ngono katika mkoa wa shinyanga na wilaya zake .

Mkuu  wa Mkoa wa Shinyanga;Ally Nassoro Rufunga,mkono wake wa kushoto anayeonekana ni Mkuu wa wilaya ya Kahama;Benson Mpesya.

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga;Ally Nassoro Rufunga,amepiga marufuku biashara ya ngono inayoshika kasi katika Halmashauri za Manispaa ya Shinyanga na ya Mji wa Kahama kwa kuziagiza mamlaka zinazohusika kufuata mkondo wa sheria dhidi ya matendo hayo.

Rufunga alitoa agizo hilo katika kikao Baina yake na Asasi zisizo za kiraia zinazojihusisha na mapambano dhidi ya maambukizi mapya ya Virusi vya Ukimwi wilayani Kahama,

ambapo alipatiwa utekelezaji wa shughuli na changamoto zinazozikabili Asasi hizo katika mapambano dhidi ya Ukimwi. Moja  wa wanaojiuza Alisema vita hivyo vya mapambano dhidi ya maambukizi mapya ya Ukimwi katika Mkoa wa Shinyanga inaathiriwa na kuwepo kwa jamii iliyojitosa kuanzisha madanguro na kufanya biashara ya ngono.

 Aidha aliziomba Asasi zinazojihusisha na miradi ya mapambano ya Ukimwi zishirikiane na serikali kwa kuyafichua madanguro hayo kisha kuwapatia elimu wajihusishao na biashara hiyo kwa kuwajengea uwezo wa kujihusisha na shughuli za ujasiriamali.

  Alizitaka Asasi hizo ziwaunganishe machangudoa katika vikundi vya kijasiriamali huku zikifanyika jitihada za kuwatafutia mitaji hatua itakayosaidia kuondokana na vitendo vyao vya biashara ya ngono na kusaidia kupunguza maambukizi ya Ukimwi.

 “Madanguro yafichuliwe,na gesti zinazofanya na kuhamasisha biashara ya ngono zichukuliwe hatua kwakuwa wanafanya jinai,”

Alisema Rufunga. Eti wapo Ofisini wakisubiri Wateja Awali Mkurugenzi wa miradi wa SHDEPHA+ wilaya ya Kahama,Venance Mzuka alibainisha kuwepo kwa biashara ya ngono wilayani Kahama kwa akiana dada wanaojiuza kukodi na kulipia vyumba kwa mwezi mzima katika baadhi ya Nyumba za kulala wageni.

“Kuna ongezeko kubwa la biashara ya ngono mjini Kahama kutokana na mji kukua kwa kasi,sababu ikiwa ni uwepo wa migodi mikubwa na midogo ya madini,huku gesti baadhi zikitumika ambazo siku zote tangu asubuhi utaambiwa vyumba vimejaa”

,Alisema Mzuka. yupo mawindoni kusaka mkate wa kila siku Mkoa wa Shinyanga hadi kufikia Juni mwaka huu ulikuwa na maambukizi asilimia 5.9 huku wilaya ya Kahama ikiwa na maambukizi asilimia 6.1 ambapo Halmashauri ya Mji ikiongoza kwa asilimia 7.8,ikifutiwa na halmashauri ya Mji wa Kahama kwa asilimia 7.8,Msalala asilimia 5.6 na Ushetu ni asilimia 5.0. Pamoja na kiwango hicho cha maambukizi imeweka mkakati kufikia mwakani 2015 uwe chini ya asilimia za kitaifa ambazo ni 5.1.

Mwisho

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply