sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» » KAMANDA MSTAAFU AONJA HARUFU YA KIFO VIPIGO VYA WAMASAI



Msimamizi mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro,Elias Kilela,akimwangalia mmoja wa majeruhi , Costa Augustino ,mkazi wa kijiji cha Dihombo wilayani Mvomero


Kamanda Mstaafu wa Polisi wa mkoa wa Pwani Ally Ambilikila na familia yake  Januari 16 alipona kufa wakati alipoonja sekseke la wafugaji jamii ya kimasai akiwa shambani akilima bonde la Mgongola kuvurugwa baada ya kuvamiwa na wafugaji hao. 

Imeelezwa kuwa kamanda huyo ni miongoni mwa wakulima 14 waliojeruhiwa na mmoja kuuawa katika balaa jingine linaloachiwa kuendelea katika mkoa wa Morogoro.

Bosi huyo wa zamani wa polisi amesema kwa mdomo wake kwamba pamoja na kukipata cha moto walimpora fedha  taslimu sh: milioni tattu na kuchomewa moto nyumba iliokuwa eneo la shamba lake. 

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro ,Leonald Paulo, alithibitisha kutokea kwa mapigano hayo na kumtaja aliyefariki ni Abdallah shomari(27) mkazi wa Msamvu Manispaa ya Morogoro ambaye alikuwa ndani ya shamba hilo na kupigwa kwa marungu na wafugaji hao.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply