sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» » » ACCESS BANK WATOA MISAADA KWA WAJASILIAMALI WAO WA MVUA YA MAWE MWAKATA

 Unga wa ugali kwa wateja wa Access Bank ambao walipata janga la mvua ya mawe katika kijiji cha mwakata vitu hivi vilitolewa kwa wateja wao walikuwa wakiishi katika kijiji hicho.
 Mafuta ya kupikia sabuni ,mchele unga wa sembe ,maharagwe ,Ndagaa ,kama jinsi vinavyonekana hapo Bank ya Access kwa ajili ya wajasilimali wao walipata majangaa ya mvua ya mawe.
Meneja wa kanda ya ziwa prosper william mwenye suti akisalimia na wahanga wa mvua ya mawe ambapo wanajasilimali hao, mwenye tishet ni meneja wa tawi la kahama Hussein kapilima ambapo wameona ni vema Bank hiyo ikawashika mkono katika kipindi hiki cha pasaka wakashiriki wote na watanzania wezao.


 meneja wa tawi la Bank ya Access mjini kahama Hussein kapilima akisoma Risala mbele ya mgeni Rasm ambaye ni meneja wa kanda prosper william kwa niamba ya mkurungezi mkuu wa Bank hiyo Roland Colon ambaye akuweza kufika katika hafla hiyo .
Baadhi ya wajasilimali wa Access Bank wanaoishi katika kijiji cha mwakata walikutwa na janga la mvua ya mawe na kupoteza zaidi ya watu 47 na majeruhi zaidi ya mia moja

 Baadha ya misaada ilitolewa na Access Bank kwa wateja wao yenye samani ya shilingi milioni moja .
Mh Diwani wa kata ya mwakata Ibrahimu six akitoa shukurani kwa niamba ya wenzeke ambao ni wajasilimali wa Bank hiyo

 Mama  salome akipokea moja ya misaada kutoka kwa kaimu mkurungezi mkuu wa Access Bank Tanzania Roland Colon ambapo yenye ni meneja wa kanda ya ziwa Prosper william.
 Mwenyekiti wa kijiji cha mwakata Ezekiel akipokea mafuta ya kupikia toka kwa meneja wa kanda wa Bank ya Access kwa wahanga wa mwakata wa mvua ya mawe .

 Pokea misaada Asante haya ni maneno ya kushukru kutoka kwa wahanga wa mwakata .
 Mama yetu mpendwa mama kalangha akipokea moja ya misaada,mafuta ya kupikia ,ndagaa mchele ,unga maharagwe , toka kwa meneja wa kanda ya ziwa ya Access Bank .
 
wakijihaada kwenda kwao baada ya kupata msaada toka kwenye  Access Bank kwa ajili ya kusherekea sikuku ya pasaka na watanzania wezao .

Nifuraha tu hapa pasaka njema kweli tunawashukuru sana Access Bank kwa msaada wao haya ndiyo maneno ya Mh Diwani wa kata hiyo Ibrahimu six akiondoka katika eneo la Bank hiyo baada ya kupokea.

Hili ndiyo Njengo la Access Bank Mjini Kahama KARIBUNI SANA WATEJA WETU .

KAHAMA
Benki ya Access tawi la Kahama  imeamua kusherehekea sikukuu ya Pasaka kwa kutoa msaada kwa wajasiriamali 11 toka kijiji cha Mwakata ambao pia ni wateja wao, waliokumbwa na janga la mvua ya mawe iliyouwa watu 47 na kujeruhi wengine 112.

Akikabidhi msaada huo Meneja wa benki hiyo kanda ya Magharibi Prosper William alisema  benki ya Access imeguswa na kilichotokea mwakata hivyo kwa kutambua umuhimu wa wateja wao wameamua kuungana kusherehekea Pasaka na wahanga hao.

Prosper amesema kushirikiana na jamii ni  moja ya wajibu wa Benki hivyo kilichowakumba watu wa Mwakata wakiwemo wateja wao kimewagusa pia na ndiyo maana wameamua kusherehekea nao Pasaka na kuahidi kuwa benki itaendelea kushiriki kwenye masuala jamii

Naye Meneja wa benki hiyo tawi la Kahama Hussein Kapilima amesema benki inabidi kubadilisha mashariti ya huduma kwa wateja hao kwani hali iliyopo kwa sasa eneo la Mwakata inawawia vigumu hata wateja wao kuyamudu masharti hayo.

Aidha  meneja wa kanda ya ziwa prosper kwa niamba ya mkurungezi wa bank hiyo Roland Colon ambaye alishindwa kufika hapo alisema kuwa nawapa pole wajasiliamali wetu kwa jangaa hili sisi kama uongozi tumeona ni vema basi kuwa shika mkono.

“Tunawashika mkono wa pole kwa tukio hilo la mwakata na kuwapatia chochote kitakajo wawezesha kusherekea vizuri pasaka pamoja na watanzania wengine.”alisema Roland colon katika taarifa yake .”

Akifafanua zaidi  mkurungezi huyo alisema pamoja na madhara hayo zipo changamoto kubwa za kimaisha zinazowakabiri ndugu zetu hawa ,likiwepo kubwa la kuhakisha wanafanikiwa sehemu ya marejesho yaliobaki kwenye mikopo yao walichukuwa kupitia Access bank alisema Roland colon.


Kwa upande wake Diwani wa kata ya Mwakata Ibrahim Six  kwa niaba ya wajsiriamali hao ameishukuru benki hiyo kwa kushiriki nao katika Pasaka na kuiomba  iendelee kuwakumbuka katika masuala mengine ikiwemo kuwapunguzia masharti katika huduma wanazozitoa.

Msaada uliotolewa na benki ya Access kwa wajasiriamali hao ambao ni wateja wa benki hiyo ni kilo 110 za Maharage,kilo 110 za Mchele,Boksi 42 za Sabuni,na Dagaa debe 22, msaada wenye thamani ya shilingi milioni
1.Mwisho


«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply