sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» » » KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YATISHIA KUFUNGA MACHIMBO MAPYA NYANG’HWALE

                      MKUU WA WILAYA YA NYANG'HWALE IBRAHIM GWIYAMA

KAMATI ya ulinzi na Usalama wilaya ya Nyang’hwale mkoa wa  Geita imetishia kuyafunga machimbo mapya yaliyoibuliwa na wachimbaji wadogo katika kijiji cha Nundu baada ya wachimbaji kumkataa mwekezaji wa kampuni ya Busolwa mining Baraka Ezekiel badala yake wanataka wafanye na kampuni ya Bismark hoteli iliyotamburishwa kwao.

Wachimbaji hao wamedai kuwa wapo tayari kufanya kazi na mwekezaji halali aliyetamburishwa kwao na serikali ambaye ni mmiliki wa kampuni ya Bismark hoteli anayedaiwa kumiliki leseni ya utafiti katika eneo hilo  na kuongeza kuwa hawapo tayari kufanya kazi na mwekezaji mwingine waliemtaja kwa jina la Baraka Ezekieli anayemiliki kampuni ya Busolwa mining anayeonekana kusimamia suala hilo.

Kamati hali isiyokuwa ya kawaida nipashe kimeshuhudia   kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya hiyo iliyoongozwa na afisa tawala wa wilaya hiyo Manyonyi Manyonyi huku jeshi la polisi likiwa limebeba siraha nzito zilizosheheni risasi za moto na mabomu ili kuweka hali ya ulinzi na usalama kwa wananchi wa eneo hilo.

 “Sisi kama wachimbaji wadogo hatuna shida na Bismark tupo tayari kufanya kazi naye lakini hali imekuwa tofauti na jinsi tulivyotarajia, kwani tunayemuona kufika mara kwa mara katika eneo letu ni Baraka anayemiliki kampuni ya Busolwa mining na amekuwa karibu sana na serikali ya wilaya  hatupo tayari kufanya naye kazi hizi  kama atakuja Bismarck mwenyewe hakuna tatizo na ni lazima tukutane naye mwenyewe hata siku zanyuma tuliambia hivi hivi huko machimbo ya Lyulu alitufukuza na sasa tumerudi hapa napo anapataka ni maelfu ya watu tupo hapa hatumtaki kabisa tumegundua wenyewe,” alisema mchimbaji aliyejitamburisha kwa jina la Elias Maliganya.

Pia wachimbaji hao wamesema kuwa kila wanapogundua madini ya dhahabu mwekezaji huyo hudai ni maeneo yake na kusababisha wachimbaji wadogo kufukuzwa na serikali  katika maeneo hayo kwa madai wamevamia leseni ya mtu jambo ambalo ni uonevu mkubwa na kunyanyaswa wachimbaji hao.

“Tunamuomba Rais Magufuri atusaidie sisi wachimbaji wadogo tuna nyanyasika kwa wawekezaji wakubwa hapa wilayani kwetu  wandishi hawa maelfu ya watu tulikuwa katika machimbo ya Lyulu ambako tulifukuzwa na huyu mwekezaji anayekingiwa kifua na serikali ya wilaya, tukakubali tukamwachia eneo baada ya kuvumbua tena dhahabu katika kijiji hiki cha Nundu kaletwa tena na serikali eti kwa kivuli cha Bismark hotel ndiyo maana tumemuomba Bismark tukutane naye lakini kama Baraka hatupo tayari,” alisema mchimbaji mwingine Mrisho Shashu.

Wachimbaji hao waliendelea kusema kuwa mwekezaji huyo waliyemtaja kwa jina la Baraka Ezekieli anajinufaisha kupitia wachimbaji wadogo kwa kudhulumu maeneo wanayovumbua wenyewe na kwamba pindi wanapogundua maeneo yenye madini ya dhahabu yeye hutumia jeshi la polisi na mkuu wa wilaya kuwaondoa katika maeneo hayo jambo ambalo wanamuomba rais kuingilia kati na kumdhibiti mwekezaji huyo.

Katika hatua nyingine mmoja wa wamiliki wa mashamba Charles Luchanganya alisema katika kikao chao kilichojumuisha wamiliki wa mashamba, Mwekezaji pamoja na mkuu wa wilaya hiyo kilichofanyika ofisini kwake walidai kulazimishwa na mkuu huyo wa wilaya kusaini makubaliano ya wao kushirikiana na mwekezaji jambo ambalo walisema hawajatendewa haki.

Akijibu malalamiko hayo wakati akizungumza na wandishi wa habari waliofika ofisini kwake mkuu wa wilaya hiyo Hamim Gwiyama alisema kuwa amepokea barua kutoka wizara ya Nishati na Madini inayoeleza kwamba Bismark ilihamisha  umiliki wake wa hizo leseni kwa kutumia sheria ya Madini  ibara no.9 hivyo ni eneo lake kwa mujibu wa Barua ya tarehe 17/03/2017.

“ Sasa kama mtu amepata haki yake kwa mujibu wa sheria utamtoa kisa jina la Baraka ama? ipo barua hapa mezani kwangu imetoka wizara ya Nishati na Madini inakwenda ofisi ya kijiji cha Lyulu Kata ya Nundu ikijibu malalamiko ya wachimbaji hao na mimi nasimamia vizuri agizo hilo,” alisema Gwiyama.

Akizungumzia kuhusu suala la kumpa ulinzi wa jeshi la polisi mwekezaji huyo Gwiyama alisema kuwa kila mtanzania anayo haki ya kupewa ulinzi isipokuwa asivunje sheria za nchi na kazi ya serikali ni kuhakikisha suala la amani linaimarika maradufu.

Kwa upande wake mwekezaji wa kampuni ya Busolwa mining Baraka Ezekiel akizungumza na wandishi wa habari alisema kuwa yeye anafanya kazi za uchimaji wa madini ya dhahabu kwa kushirikiana na kampuni ya Bismark hoteli hivyo kwa kuwa wachimbaji wamekataa kushirikiana naye ataiomba serikali ione umuhimu wa kuwaondoa hao watu waondoke kwa nguvu katika eneo hilo.

“Kinachofanyika pale kuna ugomvi wa kibiashara   kuna watu wanaojiita makota, makota hao hawa utaratibu wao huwa hawataki kufuata sheria, wao wanataka maslahi kama jana wamenunua mfuko mmoja  kwa shilingi milioni 1.2 wenye gramu 300, sawa na milioni 28 sasa hawalipi kodi mimi nitalipa kodi na nilikubali tushirikiane nao na tukawapa asilimia 60 kwakuwa wamekataa wataliacha eneo hilo,” alisema Ezekieli mwekezaji.

Naye afisa mtendaji wa kijiji cha Nundu, Juma Madinda akizungumza na wandishi wa habari waliotaka kujua uhalali wa mwekezaji huyo alisema kijiji hakimtambui kama mwekezaji wa maeneo hayo na kijiji hakina nyaraka zinazoonesha kumbu kumbu isipokuwa anafahamu hivi karibuni aliketi katika kikao cha halmashauri ya kijiji na kukosekana maelewano.

“Kama mtendaji wa kijiji husika sina nyaraka zinazoonyesha leseni japokuwa inadaiwa kuna leseni ya utafiti kwenye kijiji changu pia natambua wachimbaji wamevumbua madini kwenye mashamba ya familia mbili tofauti familia moja ni familia yam zee Luchanganya Nguguta na familia ya Mzee Emmanuel kulwa na hawa wapo zaidi ya miaka 60 sasa siwezi kumtambua wakati sijaona hata nyaraka moja na baada ya kuibuka kwa machimbo haya hakuna hata familia moja iliyoleta malalamiko kuvamiwa na wananchi wanaochimba,” alisema Madinda.

WACHIMBAJI WADOGO WAKIENDELEA NA SHUGHULI ZA UCHIMBAJI

MMOJA WA WAJUMBE WA KAMATI YA ULINZI NA USALA WILAYANI HAPA AKIJARIBU KUWASII WACHIMBAJI WALIOKUWA WAKIMKANA MWEKEZAJI WA BUSOLWA MININGI BARAKA EZEKIEL ANAYESIMAMIA LESENI YA KAMPUNI YA BISMARK HOTEL  INAYODAIWA KUVAMIWA NA WACHIMBAJI HAO.

MASHAMBA YA WANANCHI KU WALIOVAMIWA NA WACHIMBAJI WADOGO

KIKOSI CHA JESHI LA POLISI WILAYANI NYANG'HWALE KILICHOAMBATANA NA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA KIKITULIZA GHASIA KWA WACHIMBAJI WADOGO 

MMOJA WA WACHIMBAJI AKIDHIBITIWA NA JESHI LA POLISI


MWANAMKE AKICHIMBA MADINI SEHEMU WALIYO VUMBUA WENYEWE


UMATI MKUBWA WA WACHIMBAJI WADOGO WALIOVUMBUA MADINI YA DHAHABU KATIKA KIJIJI CHA NUNDU  WAKIWASIKILIZA VIONGOZI WALIOFIKA HAPO KWA LENGO LA KUWATAMBURISHA MWEKEZAJI WATAKAYESHIRIKIANA NAYE KUCHIMBA MADINI.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply