Maafisa wakuu sasa wanasema kuwa, mitambo mingine ya uchunguzi, itawekwa ambayo haitatizi pakubwa waumini wanaofika kwa maombi.
Ghasia zilizuka wakati polisi wawili wa Israel waliuawa tarehe 14 mwezi huu.
Israel ilisema kuwa mitambo hiyo ilihitajika kwa sababu watu walikuwa wakiingia na silaha katika eneo hilo takatifu.
Lakini hatua hiyo ilichochea maandamano.
Ijumaa iliyopita wapalestina watatu waliuawa kwenye ghasia na vikosi vya usalama vya Israel, wakati maefu ya waandamanaji walifika eneo la Jerusalem mashariki na ukingo wa magharibi linalokaliwa na Israel.
Israel pia inasema kuwa wafanyikazi wake wote waliokuwa wakifanya kazi katika ubalozi wake ulioko Jordan, wamewasili nyumbani, akiwemo mlinzi wa usalama ambaye alihusika katika kisa cha hapo jana Jumatatu, cha ufyatulianaji wa risasi, ambapo raia wawili wa Jordan waliuwawa.
|
habari
Habari Za Mastaa
Michezo
simulizi za kusisimua
MOHABMATUKIO.BLOGSPOT.COM's Admin
We are.., This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Post
-
Wahudumu wa kibanda kimoja cha mama lishe maarufu kwa jina la mama K wakiwa katika shughuli zao kabla ya vurumai kuanza . Weee wachet...
No comments: