sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» » » JAFO AZIAGIZA HALMASHAURI NCHINI KUWAPA KAZI VIJANA NA AKINA MAMA KWA KAZI WANAZOWEZA KUZIFANYA


Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI), Mhe.Selemani Jafo akiwa na wawakilishi wa vikundi vya vijana na kinamama wa Manispaa ya Dodoma baada ya kuwakabidhi hundi ya Sh.Milioni 70 kwa ajili ya shughuli za ujasiriamali.

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI), Mhe.Selemani Jafo akizungumza na wajasiriamali wa Manispaa ya Dodoma katika hafla ya kukabidhi hundi ya Sh.Milioni 70 kwa ajili ya vikundi vya Kinamama na Vijana.


Meya wa Manispaa ya Dodoma Profesa Davis Mwamfupe akimkaribisha Nabu Waziri Ofisi ya Rais, Selemani Jafo kuzungumza katika hafla ya kukabidhi hundi ya Sh.Milioni 70 kwa ajili ya vikundi vya kinamama na vijana.


Mwakilishi wa kikundi cha vijana akimpongeza Naibu Waziri kwa maelekezo aliyoyatoa.



Mmoja wa akinamama wajasiriamali akitoa shukrani kwa serikali baada ya kuwezeshwa.

NAIBU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, (AMISEMI), Mhe. Selemani Jafo amezitaka Halmashauri zote nchini kuwawezesha vijana na kinamama kwa vitendo kwa kuyapa makundi hayo baadhi ya kazi zilizo chini ya Halmashauri ambazo wanao uwezo wa kuzifanya ili wajiongezee kipato.

Jafo ameyasema hayo leo katika hafla ya kukabidhi hundi ya Sh. milioni 70 iliyotolewa na Manispaa ya Dodoma kwa vikundi vya ujasiliamali vya vijana na kinamama ndani ya manispaa hiyo.

Ameeleza kwamba haipendezi kwa halmashauri yeyote kuwanyima fursa ya kazi vikundi vya vijana na kinamama ambapo kazi hizo zinaweza kufanywa na makundi hayo.

Jafo ametolea mfano kikundi cha vijana cha DOYODO ambacho kina kiwanda cha kisasa cha kufyatua Matofali lakini wanahangaika soko  la kuuzia matofali wakati kuna ujenzi mkubwa wa madarasa na vyoo unaotarajiwa kuanza hivi karibuni.
“Kwa mfano kuna ujenzi unatarajia kuanza kwenye shule za msingi za Nkuhungu, Mwenge, na Ihumwa ambapo kuna zaidi ya vyumba 12 vya madarasa na vyoo matundu zaidi 18,”amesema

Naibu Waziri Jafo ameipongeza manispaa hiyo kwa kuvitumia vikundi vya vijana katika utengenezaji wa madawati ya shule za msingi na sekondari na amezitaka halmashauri nyingine hapa nchini kuiga mfano huo.


NA K-VIS BLOG, DODOMA

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply