sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» » » MAJAMBAZI WATANO WALIOFANYA MAUWAJI KIBITI WAUWAWA KAHAMA.


 kamanda wa polisi mkoa wa shinyanga Simon Haule Akionyesha siraha  ilikuwa inatumika na majambazi

 Haya ndiyo mabomu  walikutwa nayo mabomu mawili ya kutupa kwa mkono

 eneo ambalo majambazi walikuwa maficho yao

 Kamanda simon Haule akiangalia moja ya korongo la maficho ya majambazi

 Risasi, mabomu.  bunduki zilizotumika kwa uhalifu ambapo walikuwa wanakwenda kufanya shambulio

 Baadhi ya wananchi walifika chuma cha kuhifadhi maiti katika hospital ya mji wa kahama

 Wananchi wakiangalia miili ya majambazi walioletwa chumba cha kuhifadhi maiti kahama

 Moja ya siraha ilikuwa  inatumika na majambazi

 Kamanda wa polisi mkoa wa shinyanga akichungulia moja ya korongo eneo la mwanva

 Moja ya ganda  la  risasi zilizotumika kwa kurushiana  risasi

 eneo la tukio  katika chuo cha mwanva mjini kahama

 eneo la mapambano  na  damu

 Kamanda wa polisi mkoa wa shinyanga Simon Haule akiwa na mkuu wa upelezi wilaya kaham eneo la tukio ambapo majambazi watano waliuwa
WATU watano wanasadikiwa ni majambazi walihusika katika mauwaji huko katika maeneo ya Kibiti Wilaya ya Mkuranga Mkoani Pwani wameuwawa kwa kupigwa Risasi na Jeshi la Polisi Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga walipokuwa wakitaka kufanya jaribio la kuwapora wafanyabiashara wa dhahabu .

Watu hao wameuwawa juzi katika eneo la Mwanva katika kata ya Nyahanga Mjini hapa baada ya majibishano ya Risasi baina yao na Polisi wa Doria waliokuwa zamu katika eneo hilo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga Simon Haule alisema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari juzi katika Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Kahama ambapo miili ya Majambazi hayo imehifadhiwa ikisibiri kutambuliwa na ndugu zao.

Kamanda huyo alisema kuwa tukio hilo lilitokea majira ya saa tatu usiku baada ya jeshi hilo kitengo cha intelejensi kupata taarifa ya kuwa kuna majambazi ambayo yalikuwa yamejipanga kuvamia wafanyabiashara wenye maduka pamoja na wale wanajihusisha na ununuzi wa madini ya Dhahabu.

Aidha Kamanda Haule alisema kuwa baada ya polisi kupata taarifa hizo walienda katika eneo hilo ambalo lilikuwa na vichaka pamoja na mapango ambayo yalisababishwa na uchimbaji holelea wa mchanga na hivyo kuanza kurushiana Risasi kabla ya kuyazidi na kuyakamata yakiwa yamejeruhiwa vibaya.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply