sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» »Unlabelled » HALMASHAURI ZATAKIWA KUTENGA BAJETI ZA MICHEZO



Na  Mohab Dominick
Kahama
May 6, 2014.

HALMASHAURI ZATAKIWA KUTENGA BAJETI ZA MICHEZO

CHAMA cha Mapinduzi Mkoa wa Shinyanga kimezitaka Halmashauri za Mkoa wa Shinyanga kuwa zinatenga Bajeti za Michezo ambazo zitawaendeleza vijana na kuwasadia kuachana na tabia ya kukaa vijiweni bila ya kuwa na kazi ya za kufanya.

Hayo yalisemwa juzi na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga Khamis Mgeja wakati akiongea na viongozi wa Chama cha Mapinduzi kuanzia ngazi ya mashina na mabalozi katika Mji mdogo wa Isaka na kuangalia ilani ya chama hicho kama inatelezwa.

Mgeja alisema kuwa Sekta ya Michezo ni kama kazi kama ilivyo kwa kazi zingine za kimaendfeleo na kuongeza kuwa sekta hiyo ni ajira na inawasaidia Vijana kwa kiwango kikubwa katika kupambana na ugumu wa ajira hapa nchini.

“Tunaweza kukuza  ajira kwa kutumia michezo na sisi kama Chjama cha map[induzi Mkoa wa Shinyanga tunaziomba Halmashauri zote za Mkoa wa Shinyanga kuhakikisha kuwa zinaunga mkono na kusaidia vijana na katika sekta hiyo ya hichezo”, Alisema Mgeja Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga.

Aidha Mwenyekiti huyo aliendelea kusema kuwa kwa sasa Mkoa wa Shinyanga tumebahatika kupata Timu ya ligi kwa muda wa miaka 13  na kuongeza kuwa lazima tuiinge Mkono timu yetu ya Stend United kwa sasa huku tukifanya jitihada za kuzipandisha timu nyingine.

Kwa upande wake Mbuge wa Jimbo la Msalala Ezekiel Maige aliyeambatana na Mwenyekiti huyo alisema kuwa kwa sasa jimbo lake limepania kuboresha sekta ya michezo hali ambayo itakuwa ni kama ajira kwa Vijana wa jimbo hilo.

Maige ambaye alitoa kiasi cha shilingi milioni 1.4 kwa Vijana wa Kata ya Isaka kama kuunga Mkono katika kata hiyo alisema kuwa kwa sasa yupo katika mazungumzo na baadhi ya wafandhili kwa nia ya kuhakikisha kuwa Jimbo la Msalala linakuwa na timu katika kiwango cha juu.

Wakati huhuo Mbunge wa Jimbo la Kishapu Selemani nchambi alihaidi kuchagia jumla ya mipira 28 ambayo itatumika katika mashindano ya Msalala cup ambayo inatarajiwa kuanza hivi karibuni hali ambayo itakuwa ni chachu kwa viongozi wengine kuchangia katika sekya hiyo.

mwisho

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply