Baadhi ya waendesha walifika eneo la ajali kwa ajili ya kutoa huduma kwa majeruhiwi wa Roli iliokuwa linakwenda msibani baada ya kupata ajali huku watu 88 walikuwemo kwenye Roli hilo kunusurika kufa na wengine wanne kuhumia vimbaya sana.
Roli liliokuwa na waombolezaji likiwa limeanguka huku baadhi ya wananchi waliokwenda kuona ajali hiyo na kutambua ndugu na jamaa zao .
Mashuhuda wa ajali ya Roli namba T772AMQ Mali ya shija mlamu ambaye ndiye dereva wa Roli hilo ambapo likuwa na zaidi ya waombolezaji 88 ambapo wanne wao wamejeruhiwa vimbaya sana.
Askari wa usalama barabara wakikangua Roli hilo katika kijiji cha kilango wilayani kahama
Umati wa watu wakiwa na uzuni baada ya kuona baadhi ya watu walipata majeraha makubwa ktika sehemu mbalimbali za mili yao .
Askari wa usalama barabarani akijaribu kuweka vizuri usalama wa eneo hilo huku nyuma kukiwa na msururu mkubwa wa magari
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa shinyanga Khamis Mgeja akiwashukuru kikosi cha zima moto na uokoaji mjini kahama ambapo walifika eneo la tukio hilo mapema,ambapo mgeja naye alikuwa nakwenda msibani kwa marehemu mzee Timotheo ambaye marehemu mzee huyo alikuwa ni kanda wa chama cha mapinduzi ccm.
Askari wa zima moto wakitoa huduma katika ajali hiyo .
Mashuhuda wa ajali hiyo na askari wa kikosi cha uokoaji na zima moto .
Wananchi wakishuhundi ajali hiyo huku wakiwa na butwaa.
KAHAMA.
WATU 88 WANUSURIKA KUFA WAKIENDA MSIBANI NA WENGINE KUJERUHIWA VIMBAYA KAHAMA
Jumla ya Abiri 88 wamenusurika kufa baada ya Roli walikuwa
wamepanda kwenda msiba,na wengine kujeruhiwa,walikuwa wanakwenda kuzika katika
kijiji cha kilago wilayani kahama mkoani shinyanga.
Ajali hiyo imetokea katika barabara Tabora eneo la kijiji cha
kiiza kata ya kilago,Tarafa ya Dakama,ambapo gari namba T772AMQ aina ya fuso
mali ya shija mlamu (59)ambapo ndiye miliki
wa roli hilo.
Kwa mujibu wa kamanda wa polisi wa wilaya ya kahama Leonard
Nyandahu ni kweli ajali hiyo imetokea majira ya mchana saa 6 ilikuwa ilienda
msibani katika kijiji cha wame wilayani kahama ambapo watu zaidi ya 88
wamejeruhiwa katika ajali hiyo.
Aidha nipashe iliwasiliana na kamanda wa polisi wa mkoa wa
shinyanga Justus Kamugisha na kukili kuwa ni kweli ajali hiyo imetoka jana
mchana majira ya saa 6 watu hao wakikondi Roli hilo mali ya Shija mlamu(59)msukama
mkazi wa nyihongo, mjini kahama.
Kamanda kamugisha aliwataja watu walijeruhiwa vimbaya katika
ajali hiyo wanne kati yao hali zao ni mbaya ni Elizabeth shabani (32)msukuma
mkazi wa nyihongo ambaye amevujika mkono wa kulia 2. john Timotheo (39)msukuma mkazi wa
nyihongo ambaye amevujika mguu wa kulia 3.Elias majani (50)msukuma mkazi wa
ngaya ambaye hajitambui mpaka sasa 4.mwanamke
moja hajajulikana jina wa mkazi yake( 33)ambaye amekatwa mkono wa kushoto.
Aidha kamanda Justus majeruwi wengine wana majeraha ya
kawaida wanaendelea kutibiwa na kuondoka
mpaka sasa majeruhi waliopo hospitali ya wilaya ni 25 kati yao wanaume 6
na wanawake 19hali zao zinaendelea vizuri.
Aidha kwa upande wake Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya wilaya ya kahama Dr Athumani hussen
Alisemakuwa walipokea jumla ya majeruhi 88 kati yao wanawake walikuwa 66 na
mtoto moja wakike ambapo mjula yao wanakuwa 66 na wanaume walikuwa 22 kati hao
wanne hali zao zilikuwa mbaya sana na kusema kuwa mwanamke moja alikuja
kungundulika majira ya usiku na kujua hali yake ilikuwa mbaya zaidi baada ya
kuchukuwa vipimo alingudulika kuwa tumboni kwake Badama ilikuwa ilimepasuka
alisema DR Athumani.
Dr Husseni Akilifafanua alisema kuwa wagonjwa wengine ndugu
zao waliwachukuwa na kuwapeleka katika hospitali ya Rufaa ya kinga wilayani
Nzega mkoani Tabora kwa Matibabu zaidi ,ambapo alikuwa na majeraha makubwa.
Kamugisha alisema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa
Dereva wa gari hiyo pia ni miliki wa Roli hilo shija mlamu 59 mkazi wa nyihongo
wilayani kahama,kesho hatafikishwa kahama baada ya uchunguzi kukamiliki kujibu
mashataka ya kuendesha gari kwa uzembe.
Mwisho
No comments: