sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» » » DC AWAWEKA NDANI MAAFISA AFYA KWA KOSA LA KUKAIDI AMRI YAKE

 Uchafu ambao unazangaa katika mji wa kahama ambapo  mkuu wa wilaya ya kahama Fadhili Nkulu amepinga marufuka katika kata zote za halmashauri ya mji wa kahama kama njisi unavyona  uchafu huo katika nyumba ambazo zipo karibu na uchafu.  

 Mwenyekiti wa Wa Mtaa wa Majengo mama Sumuni akiangalia uchafu jinsi wakazi wa kata ya majengo wakitupa bila utaratibu eneo hili sasa limekuwa ni hatari kubwa kwa kazi wa maeneo ya  majengo 

 Hili ndiyo GUBA la kata ya majengo ambalo wakazi wake awana ustarabu wa kutupa taka humo katika guba hilo kama jinsi linavyonekana kwa bali hicho kibanda  kama njisi kinavyonekana kwa mbali 

Uchafu na njia 

Uchafu baadhi ya maeneo ya kahama mjini 

Uchafu 

Eneo ambalo linaoyesha linaonyesha kibao cha barabara kuu ya kuingia katika mji wa kahama na kulekea nchi za Rwanda, Burundi na kongo ambapo mkuu wa wilaya alisema ndiyo jicho la mji wetu  

 Mkuu wa wilaya ya kahama DC Fadhili Nkulu Akiongea na waandishi juu ya uhamuzi wake wa kuweka rumande Mtendaji wa kata na Afisa Afya wa Mji


KAHAMA

 
MKUU wa Wilaya ya Kahama Fadhili  Nkulu amewaweka mbaroni Maafisa afya wa Halmashauri ya Mji wa Kahama kwa kosa la kuacha uchafu ulikokuwa katika Barabara kuu ya Mji wa Kahama ya  kwenda katika Nchini za jirani za Rwanda na Burundi hali ambayo imesababisha eneo hilo kuwa mrundikano mkubwa wa taka  zilizokuwa zikitoa harufu mbaya.

Maafisa Afya hao waliowekwandani na Mkuu huyo wa Wilaya ni Johanes Mwebesya  na mtendaji wa kata  ya nyasumbi   Enocent kapeli  kwa kosa la kutoa uchafu hulioko mwanzo wa barabara kuu ya kuingia katika mji wa kahama eneo la Phatom na  kuacha wanachi wakitupa taka katika eneo hilo ambalo halistahili.

Tukio hilo limetokea  jana wakati Mkuu wa Wilaya ya Kahama
Fadhili Nkulu akipita eneo la phatom  akielekea halmashauri ya ushetu kwa ajili ya ziara ya kikazi za kawaida na kuona lundo la uchafu katika barabara hiyo  kuu ya kuingia Kahama Mjini jambo ambalo linalita sura mbaya kwa mji wa Kahama.

Aidha Mkuu huyo wa Wilaya Fadhili  Nkulu alisema alitoa maagizo kabla ya kuondoka kwenda Halmashauri ya Ushetu  mbele ya Mkurungezi wa Halmashauri ya  Mji wa Kahama Anderson Msumba pamoja na Mtendaji wa kata hiyo na afisa afya wa kata hiyo kuwa akirudi kutoka Ushetu akute  uchafu huo umeondolewa hapo haraka sana jambo ambalo halikutekelezeka.

Nina waambia nyinyi maafisa Afya  nikirudi toka ushetu  jioni nikute lundo hilo la chafu limeondoka eneo hilo na pawe safi sitaki kuona takataka katika eneo hilo kwani hapo ni katika sura ya Wilaya ya Wilaya hata mgeni akija katika Mji wa Kahama cha kwanza kuona ni uchafu uliopo eneo hilo”, Alisema Mkuu huyo wa Wilaya ya Kahama Fadhili Nkulu.


“Watumishi hawa wa Halmashauri ya Mji wa Kahama Wamezoea kufanya kazi kwa mazoea jambo ambalo limekuwa ni kero kwa wananchi haiwezekani mwanzo tuu wa kuingia Mjini wa Kahama  kunakutana na  Dapo la uchafu je huko ndani kutakuwa na hali gani kama mwanzo tu kunakuwa na Mrundikano wa taka kiasi hicho.”Alisisitiza Mkuu huyo wa Wilaya.

Hata hivyo alisema kuwa wito wake kwa sasa kwa watumishi wa umma ni kuacha mara moja kufanya kazi kwa mazoea na kuakikisha kila moja wetu anatunza maeneo yake ya kazi  na kufanya  usafi katika maeneo yaliomadhubuti kwa hali ambayo itachangia kiasi kikubwa kuuweka Mji wa Kahama katika hali ya usafi hali ambayo inaweza kuchangia katika kuzuia magonjwa ya milipuko kama pikindupindu .

Mkuu huyo wa Wilaya ya Kahama Fadhili Nkulu pia aliwataka Watumishi wa Serikali kuacha kufanya kazi kwa mazoea kwani Serikali hii ya awamu ya tano chini ya Rais John Pombe Magufuli na kauli yake ya hapa kazi inatakiwa kila mtumishi ajitume katika kufanya kazi za kuwahudumia Wananchi hali ambayo italeta mabadiliko makubwa katika utendaji wa kazi.

Mwisho



«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply