|
Moja ya Darasa ambalo ilimejengwa kwa msaanda wa mgodi wa buzwagi huku nguvu za wananchi zikiwa zimetupiliwa mbali kama jinsi matofari 2300 ambyo wanakijiji wa Budushi walinunua kwa fedha zao. |
|
Two in one nyumba za walimu mpya katika shule ya msingi Budushi |
|
Vyoo vya shule ya msingi Budushi ambapo kuna matundu 32 kwa wavulana na wasichana |
|
Moja ya jengo la Madarasa ya shule ya msingi Budushi kata ya mwendakulima kati |
|
Mbunge wa jimbo la kahama Jumanne kishimba akiwa na Afisa Elimu wa shule za msingi Aluko Lukolela Mwenye kitabu cha blue wakisubiri ufunguzi wa shule hiyo toka katika uongozi wa mgodi wa buzwagi |
|
Mafundi wakikamilisha ufungwaji wa madirisha katika baadhi ya madarasa katika shule hiyo ya Budushi |
|
Eng. Asa Mwaipopo pia ni meneja wa mgodi wa Buzwagi akitolea maelezo juu ya ujenzi wa shule hiyo kwa mkuu wa wilaya ya kahama Fadhili Nkurlu katika kijiji cha Budushi wilayani kahama mwenye kofia nyeupe ni mkuu wa wilaya ya kahama |
|
Mwenyekiti wa Halmashauri ya mji wa kahama Abel shija wakiangalia ujenzi wa shule hiyo |
|
Mkuu wa wilaya ya kahama Fadhiri Nkurlu na Mbunge wa jimbo la kahama mwenye upara nyuma ya Dc jumanne kishimba kuli ni kaimu kurungezi wa mji |
|
Eng. Asa mwaipopo akimuonyesha mkuu wa wilaya ya kahama Fadhili Nkurlu moja ya madarasa mwenye miwani na kofia nyeupe |
|
Mkuu wa wilaya ya kahama Fadhili Nkurlu Akinywa maji salama katika kisima kilichojengwa na mgodi huo wa buzwagi katika shule ya msingi Budushi |
KAHAMA
Baadhi ya viongozi wa Kijiji cha Budushi kata ya Mwendakulima
wilayani Kahama mkoani Shinyanga wameulalamikia Mgodi wa Madini wa Acacia
Buzwagi kwa kufanya mambo kijijini humo bila kuwashirikisha wananchi,ambao
walianzisha ujenzi huo.
Akizungumza kabla ya zoezi la kukabidhiana Shule ya
Msingi Budushi yenye vyumba 6 vya madarasa, ofisi mbili na nyumba moja ya
walimu, Mtendaji wa Mtaa wa Mwendakulma Kati Christopher Laurent amesema
mradi huo uliibuliwa na wananchi wenyewe na kuanza hatua za ujenzi kabla ya
kupata ufadhili kutoka mgodi wa Buzwagi.
Alisema tangu mgodi huo ufadhili ujenzi wa shule hiyo wananchi
wamekuwa hawashirikishwi katika shughuli za ujenzi huo jambo ambalo ni
kuwatenga waanzilishi wa mradi huo kutokana na wanafunzi wa kijiji hicho
kulazimika kutembea umbali mrefu kufuata Elimu vijiji jirani.
Naye Mwenyekiti wa Mtaa wa Mwendakulima Kati Abdulrahman
Abdallah baada ya wananchi kuanzisha mradi huo kisha kufadhiliwa na Mgodi wa
Acacia Buzwagi lakini Halmashauri ya Mji wa Kahama haijachangia chochote ili
kuwaunga mkono wananchi walioanzisha ujenzi huo.
No comments: