By: Mohab Dominic
on 01:43
/
|
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP
Saimon Sirro, amefanya mabadiliko ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni
pamoja na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Shinyanga.
Katika mabadiliko hayo, aliyekuwa
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa
Polisi (SACP) Suzan Salome Kaganda amekuwa Mkuu wa kitengo cha Mafao na Fidia
Makao Makuu ya Polisi, na nafasi yake inachukuliwa na Kamishna Msaidizi
wa Polisi (ACP) Murilo Jumanne Murilo ambaye alikuwa kamanda Polisi Mkoa wa
Shinyanga.
Aidha, Nafasi ya aliyekuwa Kamanda wa
Polisi Mkoa wa Shinyanga imechukuliwa na Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP)
Simon Sylverius Haule, ambaye alikuwa Afisa Mnadhimu wa Polisi wa Mkoa wa
Mara.
Uhamisho huo ni mabadiliko ya kawaida
yanayotokea ndani ya Jeshi la Polisi katika kuongeza ufanisi wa utendaji
kazi.
Imetolewa na:
Barnabus D. Mwakalukwa - ACP
Msemaji wa Jeshi la Polisi.
Makao Makuu ya Polisi.
|
Tag:
habari
matukio
MOHABMATUKIO.BLOGSPOT.COM's Admin
We are.., This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
No comments: