sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» »Unlabelled » WADAU WAOMBWA KUSADIA SHULE ZA WAZAZI



Na 
Kahama
Jan 24, 2014.
 

WADAU mbalimbali wa Elimu wakiwemo wazazi Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga wametakiwa kujitokeza kwa wingi katika kusaidia Shule za sekondari zinazomilikiwa na Wazazi baada ya shule hizo kuonekana  zinapoteza mwelekeo kutokana na kukosa vifaa mbalimbali vya kielimu.

Hayo yalisemwa juzi na Kaimu Meneja wa Shirika la Hifadhi ya Jamii Mkoa wa Kahama ( NSSF) Ernest Rusato wakati akikabdhi Vitanda 80 na Magodoro ya idadi hiyo kwa Katibu wa umoja wa Wazazi wa CCM Wilayani Kahama Sharon Tulliy kwa ajili ya kusadia katika shule ya sekondari ya Wigehe inayomilikiwa na Wazazi.

Rusato alisema kuwa Shirika lake lilipokea maombi ya msaada wa Vitanda pamoja na Magodoro kutoka kwa uongozi wa Wazazi wa CCM wenye thamani ya shilingi milioni 30 lakini kusadia kwa kiasi kidogo wameamua kutoa msaada huo wenye thamani ya shilingi milioni 10 vyote kwa pamoja.

Aidha Kaimu meneja huyo aliendelea kusema kuwa NSSF mbali ya kujihusisha katika shughuli mbalimbali za kujenga uchumi hapa Nchini pia wanajuhususha katika kutoa misaada mbalimbali hasa katika sekta mbalimbali ikiwemo ile ya kukuza Elimu hapa nchini.

Pia aliwataka Wanafunzi wa Shule hiyo kpitia msaada huo kuhakikisha kuwa wanasoma kwa bidii zaidi kwani wazazi wao wanajinyima kwa kugharamikia karo za shule hali ambyo itawatia matumaini na hivyo kuweza kutimiza ndoto zao walijiwekea hapo siku za baadaye.

Kwa upande wake katibu wa Wazazi wa CCM Wilaya ya Kahama Sharon Tulliy alisema kuwa msaada huo umekuja wakati muafaka kwani shule yake ilikuwa ikihitaji jumla ya vitanda 100 na kugeza kuwa sasa limebakia pengo la vitanda 20 tuu katika shule hiyo ya Bweni yenye Wanafunzi 484 wa kike na kiume.

Tulliy alisema Shule hiyo ambayo ni mali ya umoja wa Wazazi Tanzania inatoa huduma za utaalamu na ina sifa nzuri pia haiendeshwi kibiashara hali inayofanya kila mtoto mwenye kuwa na uwezo wa kusoma katika shule hiyo bila ya kuwa na masharti yeyote yale.

Pia Tulliy aliwataka wadau wengine mbali na shirika hilo la Hifadhi ya jamii kujitokeza kwa moyo katika kusadia shule hiyo ambayo kwa ujumla baadhi ya wasomi wengi wa Wilaya ya Kahama wamesoma katika shule hiyo akiwemo Mbunge wa Jimbo la Kahama James Lembeli pamoja na Jaji mstaafu Hiema.

Shule ya Sekondari ya Wigehe ilianzishwa Mwaka 1954 kama shule ya ufundim kabla ya mwaka 1984 kuwa sekondari inahitaji msaada wa haraka kutokana na uchakavu wa majengo yake pamoja na mabweni ya kulala wanafunzi hali ambayo wadau na watu wenye mapenzi mema hawana budi kuisaidia shule hiyo.

mwisho

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply