Na
Mohab Dominick
Geita
Febr 28,2014.
mwanamke Moja Christina
Charles (20) mkazi wa Kharumwa mkoani Geita amefariki dunia akiwa
Guest(Nyumba ya kulala wageni) akiwa na mpenzi wake Mniry Masii mfanyakazi wa
kituo cha afya cha Kharumwa katika halmashauri ya wilaya Nyang’hwale mkoani
Geita.
Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia
jana katika Nyumba ya kulala wageni iliyopo mjini Nyang’wale
inayojulikana kwa jina la Saju Guest house.
Imedaiwa kuwa siku hiyo mtuhumiwa
ambaye ni mfanyakazi wa kituo hicho cha afya ambaye ni katibu wa kituo
cha afya Kharumwa anayefahamika kwa jina la Mniry Masii alimchukua
Christina Charles(20) ambaye ni mkulima muda wa saa tatu usiku na kwenda naye
katika gesti hiyo na kupewa chumba kwa ajili ya kupumzika.
Habari zinasema kuwa ilipofika
saa 7 usiku mhudumu wa gesti hiyo aliitwa na (Mniry Masii) mtuhumiwa huyo aende
kwenye chumba chake na alipofika alimkuta huyo mama anatoa mapofu na mtuhumiwa
akiwa amekaa pembeni huku akilia....
Mhudumu alipomuuliza
mwanamme(Mniry Masii) kulikoni!! ,hakujibu chochote zaidi ya kuendelea kulia
kutokana na kutojibiwa yule mhudumu alirudi alikokuwa.
Imeelezwa kuwa mhudumu huyo wa gesti
aliporudi na kulala baada ya muda mfupi tena akaitwa tena na bwana
Mniry Masii akasema kuwa mpenzi wake Christina amebanwa na kifua ,ndipo
wakambeba na kumpeleka hospitali ya Kharumwa na walipofika tayari alikuwa
amefariki dunia.
Diwani wa kata ya Kharumwa Marco Masusu
amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa tayari mazishi
yameshafanyika.
Hata hivyo inadaiwa kuwa mwanamke
huyo enzi za uhai wake alikuwa na matatizo ya kuugua kifua na baadhi ya
watu wamesema kuwa huenda hali ya hewa kulingana na tatizo hilo imepelekea
kuweza kupoteza maisha katika hali aliyokutwa nayo.
Naye mama mzazi wa marehemu Bi, Salome
Nkuji (30) ambaye ni mkazi wa Mwanza alipofika msibani alieleza kuwa binti
yake alikuwa na matatizo ya muda mrefu tangu azaliwe.
“ Binti yangu tangu nimzae miaka 20
iliyopita alikuwa na tatizo la kifua (athma)’’ ,alisema mama huyo bila ya
kuongeza lolote.
Kaimu kamanda wa polisi mkoani Geita
Simon Pasua amethibitisha kuwepo kwa tukio hilo na kuongeza kuwa Mniry Masii
(mtuhumiwa ) hajatenda kosa la kuua bali ni hali ambayo imetokea kama ambavyo
mtu anaweza kuwa amelala na mtu mgonjwa halafu mauti yakampata .
“Ndugu mwandishi ni kweli tukio lipo
lakini haya sio mauaji ni mtu ambaye alikuwa anaumwa siku zake zimefika
kwa hali hiyo na tulimshikilia mtuhumiwa tumemhoji na tayari
tumeshamwachia”,alisema kamanda Pasua.
MWISHO
No comments: