sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» »Unlabelled » DIWANI APINGA UANZISHWAJI WA MAENEO MAPYA YA UTWALA BUKOMBE



Na  Mohab Dominick
     Bukombe
    March 18, 2014 

DIWANI APINGA UANZISHWAJI WA MAENEO MAPYA YA UTWALA BUKOMBE.



MKUTANO maalumu wa balaza  la Madiwani  wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita  nusula  ushindwe kufikia  maazimio  baada ya mmoj wa Diwani  kutoka katika chama cha  Upinzani  Soud Ntanyagara  (CHADEMA) Kupinga uanzishaji wa maeneo mapya ya utawala .

Mkutano huo maalumu  wa balaza  ulioketi  hivi karibuni  katika ukumbi wa Halmashauri ya  Wilaya ya Bukombe  uliokuwa na lengo la  kupitisha mapendekezo  ya uwanzishwaji  wa maeneo mapya ya utawala ikiwa ni pamoja na vitongoji vipya, Vijiji pamoja na kata.

Akifungua  mkutano huo mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya  ya Bukombe   Felix Kulya  aliwaarifu  wajumbe  kuwa  ajenda  iliyopo katika Baraza hilo  ni kupitisha  mapendekezo yaliyowasilishwa mbele ya balaza na si vinginevyo .
Alisema Agenda hizo zilikuwa muhimu kupitishwa kwani mchakato ulikuwa umeanza na lilikuwa agizo toka juu  ambalo halikupaswa  kujadiliwa bali kutekelezwa tuu na baraza hilo la Madiwani .


Akichangia  hoja katika  balaza hilo  diwani  wa kata ya Igulwa (CHADEMA)  Soud Ntanyagara  alitaka kujua  jografia  na hali ya uchumi  katika Wilaya  endapo inaweza kugharamia watendaji na  viongozi  watakao hitajika katika  maeneo hayo mapya  ikiwa  hata yale yaliopo  miundo mbinu yake ina sua sua.
 Ntanyagara alisema kuwa  kwa sasa zaidi ya  watendaji wa kata na vijiji  wapatao 40 wanafanya kazi kwa kujitolea katika ngazi  husika pamoja na hayo Halmashauri bado  haijakamilisha ujenzi wa  Zahanati   kwa kila kijiji  na  vituo vya  afya kwa kila Kata.

Pia Diwani huyo alisema kuwa baadhi ya vijiji  havina shule   za msingi na sekondari  pamoja na miundombinu  ya mawasiliano  yaani barabara  za kuunganisha kijiji na kijiji kata na kata  na makao makuu ya Halmashauri ya Wilaya hali ambayo inakuwa ni vigumu katika suala zima la utekelezaji wake .

“  Tusijibebeshe mlima  wakati  tumeshindwa kubeba kichuguu,  hivyo  nauliza mwenyekiti   hali ya mapato  ya  ndani  kwa Halmashauri yetu  ikoje  kwakuwa  hata barua niliyonayo mkononi ya wito wa balaza  la leo  imeonyesha  mwendelezo wa mazoea  kwa  waheshimiwa  na wataalamu  kukopwa posho za vikao  kwa maelezo kuwa Halmashauri  ina  hali ngumu  kimapato na  iweje  tushindwe  kulipa  posho ya madiwani 18  halafu  tuongeze kata”, Alisema Diwani huyo.   

Hata hivyo Mwenyekiti wa Halmashauri  hiyo Kulya  alitoa angalizo  kuwa   haitakuwa sahihi  kwenda kufanya  mikutano  na wananchi  kupinga  mchakato huo  kwa kuwa  yalikuwa  bado ni  mapendekezo ambayo.

Vuta ni kuvute hiyo  ilidumu  zaidi ya masaa matatu  mvutano kati  ya  Soud Ntanyagara ,  Patric Kagulusi na Mwenyekiti wa Halmashauri  Joseph Kulya  huku madiwani waliosalia  wakipiga  meza  kumsisitizia  mwenyekiti  kupitisha  azimio.

MWISHO.


«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply