sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» »Unlabelled » WAKULIMA WA TUMBAKU KUWA BIMA



Na  Mohab Dominick
Kahama
May 25, 2014.

WAKULIMA WA TUMBAKU KUWA BIMA

KAMPUNI ya Real Insurance Tanzania Limited kwa kushirikiana na Benki ya CRDB iko mbioni kutoa Bima kwa ajili ya Wakulima wa zao la Tumbaku Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga  kwa lengo la kuwafanya wakulima hao waweze kukopesheka katika sekta ya Kilimo.

Akiongea katika Mkutano Mkuu wa Chama cha Ushirika Wilaya ya Kahama (KACU) Meneja wa Kampuni hiyo Sodson Manatsa alisema kuwa Kampuni yake itatoa Bima hiyo ya kinga ya majanga ya mvua, Upepo pamoja na mambo mengine kwa Mkulima.

Manatsa alisema kuwa Wakulima wa zao la Tumbaku itakuwa ni muda muafaka wa kujiunga na bima hiyo kwa Bei ya Chini huku kila Mkulima akitozwa asilimia 1.5 kwa  ya mavuno yake aliyoyapata kwa msimu ulipo wa zao hilo.

Alisema kuwa hapo siku za nyuma wakulima walikuwa ni wagumu katika suala zima la kupata mikopo kutoka katika asasi mbalimbali za kifedha kutokana na kutokuwa na kinga yaani bima na kungeza kuwa kwa wakati huu itakuwa ni niia nyepesi kwao katika kuchangamkia fursa za mikopo.

Hata hivyo akiendelea kutoa maelezo juu ya bima hiyo Meneja huyo alisema kuwa katika kuhakikisha Wakulima wa zao la Tumbaku wanakuwa ni bima hiyo ya mzao wataanza kupita katika vyama mbalimbali vya msingi kwa nia ya kutoa Elimu na Semina ili Wakulima waweze kujua faida ya kuwa na Bima ya mazao.

Alisema kuwa suala hilo la Bima ya Tumbaku halitawahusisha Wakulima na Makampuni yao ya ununuzi bali ni kwa Mkulima yeyote ambaye analima zao la Tumbaku jambo ambalo wakitumia vizuri itawatoa katika wimbi la umasikini na kuweza kupata mikopo sehemu mbalimbali.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Ushirika Wilaya ya Kahama (KACU) Said Tangawizi alisema kuwa wao kama Wakulima wa Tumbaku jambo hilo wamelipokea na watalichukulia kama makisio  na kisha kulitolea maamuzi baadaye.

“Suala la kuanzishwa kwa Bima ya zao la Tumbaku sio baya kwa Wakulima bali lisiangaliwe kwa upande mmoja na lisiingizwe katika utekelezaji kwa sasa ili wakulima waweze kulitafakari wakati wakiwa wanapewa semina na Elimu juu ya Bima hiyo”, Alisema Tangawizi Mwenyekiti wa Chama cha Ushirika Wilaya ya Kahama (KACU).

Chama cha Ushirika Wilaya ya Kahama juzi kilifanya mkutano wake Mkuu wa kumi na nane wa mwaka kwa lengo la kujadili mambo mbalimbali yanayohusu Ushirika huo ikiwa ni sambamba na mapato na matumizi, faida na madeni mbalimbali yaliopo katika ushirika huo ambapo unajumuisha Wajumbe kutoka katika Wilaya ya Kahama, Bukombe, Biharamulo, Chato pamoja na Geita.

Mwisho.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply