Mkuu wa wilaya ya kahama Benson Mpesya Akiwa na Mkurungezi Mtendaji wa Kampuni ya Afrrican Barrick Gold Mine Brad Gordon mwenye kitambulisho cheupe wakati wa ukanguzi wa barabara za mji wa kahama Ambao umefadhiliwa na Mgodi wa Buzwangi kwa kiwango cha Lami kwa Gharama ya bilioni 3
Mkuu wa wilaya ya kahama Benson Mpesya ambaye anaonyesha mkono Mkurungezi Mtendaji wa kampuni ya Afrrican Barrick Gold Mine Brad Gord ujenzi wa Barabara ya Lami Mjini kahama (ABG)
Mmoja ya mitaa ya mji wa kahama Ambayo ipo katika kiwango cha lami huu ni moja wa mtaa wa igalilimi
Afisa Mahusiano wa Mgodi wa Buzwangi Moses Msofe mwenye shati nyeupe Akimsikiliza mkuu wa wa wilaya kahama.
Mkuu wa wilaya ya kahama Benson Mpesya mwenye suti nyeusi wa kati Mkurungezi Mtendaji wa kampuni ya Afrrican Gold Brad Gordon mwisho kulia ni Meneja wa Mgodi wa Buzwangi Philiber Rweyemamu na nyuma ni jamal Rwambo mwenye shati la mistali .
Mmoja ya mifereji ambayo ipo kati kati ambazo zinajengwa kwa kiwango cha lami mjini kahama
Mkuu wa wilaya kahama Benson Mpesya Akiongea na Waandishi wa habari Hawapo pichani
Mkuu wa wilaya kahama Benson Mpesya Akiwa na Mkurungezi Mtendaji wa Kampuni ya Afrricani Barrick Gold Mine Wakiwa ofisi kwake leo kwa ajili ya kuona Mradi wa barabara za mji wa kahama kwa kiwango cha Lami ambao ujenzi huu hutachukuwa muda wa miezi 6
MKuu wa wilaya ya kahama Benson Mpesya Akisisitiza jambo leo na uongozi wa Afrrican Barrick Gold mine Hawapo pichana
Mmoja ya Barabara za Mji wa mji wa Kahama Ambazo zilivyo sasa baada ya kuwekewa Lami
Mkurungezi Mtendaji wa Afrrican Barrick Gold Mine Brad Gordon Mwenye Kuonyesha ubora wa Barabara jinsi zilivyojengwa kwa kiwango cha Lami mwenye Tsheti ya Blue ni Meneja wa Mgodi wa Buzwangi Philiber Rweyemamu .na mwenye shati jeupe ni muandishi wa habari wakipokea maelenzo
Mkurungezi Mtendaji wa Afrrican Barrick Gold mine Brad Gordon na Meneja wa Mgodi wa Buzwangi Philiber Rwayemamu picha zote na Mohab Dominick
KAMPUNI ya ya African Barrick Gold Mine inayomiliki Migodi ya dahabu ya Bulyanhulu na Buzwagi imetumia jumla ya Shilingi Bilioni 64 katika shughuli mbalimbali za maendeleo ya jamii kwa jamii inayozunguka Migodi hiyo Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo Brad Gordon alisema Kampuni yake imetumia fedha hizo katika kuibua miradi mbalimbali ya maendeleo kwa Wananchi wanayozunguka Migodi hiyo katika sekta mbalimbali za Elimu, Afya, Maji pamoja Michezo kwa lengo la kuharakisha maendeleo na ustawi wa jamii.
Hayo aliyasema wakati wa ukaguzi wa barabara zanye urefu wa zaidi ya Kilometa sita zinazojengwa kwenye mji wa Kahama kwa kupitia ufadhili wa Kampuni hiyo ya African Barrick Gold kwa kushirikiana na Serikali kwa lengo la kupunguza adha ya vumbi na ubovu wa barabara zilizokuwepo awali.
Alisema kampuni hiyo imeamua kushirikiana na serikali kujenga miundombinu hiyo ili kuiwezesha jamii kuwa karibu na migodi yake na kuondoa dhana iliyokuwa imezoeleka kuwa wawekezaji hawanafaida yoyote kwa wananchi na kuwa itaendelea kutengeneza miundombinu mbalimbali katika maeneo hayo ili kuharakisha maendeleo na kukuza uchumi wa wananchi.
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Kahama Benson Mpesya alisema mji wa Kahama unakuwa kwa kasi kutokana na shughuli za madini zinazofanywa na migodi hiyo miwili mikubwa ya Bulyanhulu na Buzwagi na hivyo inahitaji mipango ya haraka kuuwezesha kuwa na miundombinu muhimu kama vile barabara za lami, taa, na mifumo mizuri ya kutiririsha majitaka.
Alisema serikali inatambuaumuhimu wa uwepo wa wawekezaji katika kusaidia shughuli muhimu za maendeleo na hivyo kuitaka jamii kushirikiana nao badala ya kuwabeza hawarudishi faida wanayoipata kwa ajili ya maendeleo yao.
Aliongeza kuwa serikali itahakikisha inasimamia sera yake ya uwekezaji na kuwahakikishia usalama wawekezaji hao ili wafanye kazi zao kwa amani na utulivu kwa lengo la kusogeza mbele gurudumu la maendeleo ya taifa.
Kampuni ya African Barrick Gold (ABG) imetumia zaidi ya shilingi Bilioni 3.2 kwa ajili ya ujenzi wa barabara hizo za kiwango cha lami zinazozunguka mji wa Kahama huku mchango wa serikali katika ujenzi wake ikiwa ni shilingi Milioni 700 kutoka ofisi ya waziri mkuu.
No comments: