MADIWANI
wa Halmashauri ya Wilaya ya msalala wamepinga Mapendekezo ya kitengo Idara ya
Afya kuongeza kiasi cha fedha za huduma za papo kwa papo kutoka kiasi cha
shilingi 1,000 kilichokuwepo hapo awali hadi kufikia kiasi cha shilingi 7,000
kwa lengo la kuchangia mfuko wa afya ya jamii (CHF).
Diwani
wa viti Maalum (CCM) Angela Paulo kutoka kata ya segese alikuwa wa kwanza
kupinga mapendekezo hayo yalioletwa katika Baraza la Madiwani na Kaimu Mganga Mkuu wa Haspitali wa Halmashauri
hiyo Charles Kalidushi na kuongeza kuwa kwa kufanya hivyo ni kama kumuongezea
Mwananchi mzigo.
Paul
alisema kuwa kwa sasa Wananchi wanashindwa kumudu kuchangia huduma ya shilingi
1,000 katika kupata huduma Hospitali ya Wilaya na kungeza kuwa kwa kitendo cha
kungeza fedha hiyo kutawapa shida wananchi na kunaweza kuchangia kuongzeka kwa
vifo hasa kwa akinamama.
“Kitendo
cha kuongeza malipo ya huduma za papo kwa papo katika Hospitali ya Wilaya ni
kitendo cha kumuongzea Mwananchi mzigo kwani hiyo ya awli tuu hawezi kumudu na
mkifanya hivyo mnaweza kuongeza vifo hasa kwa jamii ambayo haina uwezo wa
kumudu gharama hizo”, Alisema Angela Paul.
Aidha
Diwani huyo alisema kuwa njia ya kuwafanya wananchi kuingia katika mfuko huo wa
Afya ya jamii kwa kuwaongezea huduma hiyo ni bora wakaelimishwa kwanza kabla ya
kujiunga na mfuko huo huku wataalamu wa Idara ya Afya wakishirikina na madiwani
kupita katika kata mbalimbali kwa lengo la kuwashawishi wananchi juu ya mfuko
huo.
Awali
akitoa Mapendekezo hayo Kaimu Mganga Mkuu Halmashauri ya Masalala Charles Kalidushi
alisema kuwa Idara ya afya imeamua kutoa mapendekezo hayo kwa madiwani hao
ili iwe rahisi kwa Wananchi kuchangia
kiasi hicho cha fedha ili waweze kupata huduma wao na familai zao.
Kalidushi
maliendelea kusema kuwa tayari watu wa idara ya afya wameishaanza kupita
vijijini kwa lengo la kuwaelewesha wananchi juu ya umuhimu wa kuingia katika
Mfuko wa Afya ya jamii na wananchi wameonyesha nia ya kuchangia kiasi hicho cha
fedha cha shilingi 7,000 kwa mwaka.
Alisema
kuwa kwa kupitia Mfuko wa Afya ya jamii (CHF) Wananchi hawatakuwa na shida ya
kupata Dawa katika Vituo vya Afya sambamba na kulipia kumuona daktari hali
ambayo itakuwa rahisi kwa kupata huduma haraka na kuwahi kurudi majumbani kwao
mapema kuliko ilivyokluwa awali.
Mwisho.
No comments: