UMOJA wa
wazee (UWAKA) katika halmashauri ya mji
Kahama umelalamikia Madiwani watatu Bobson Wambula (CHADEMA) Majengo James Mlekwa (CCM) Nyahanga na Mussa Mabubu (CCM) Busoka kwa kudaiwa kuchukua sh.480,000 posho ya ziara ya Mbeya kujifunza
usafi.
Wakizungumza
katika kikao chao wazee hao, walisema kitendo walichokifanya Madiwani hao ni
kuwadhulumu wananchi kwani fedha waliyochukua jumla ya shilingi 1440,000 na
kuacha kwenda ziara ingesaidia kujenga hata
chumba kimoja cha ofisi ya zima moto
kutokana na kikosi hicho kukosa ofisi.
Akizungumzia
kero hizo katika kikao hicho kilichofanyika katika Hoteli ya Rockpoint mjini
Kahama katibu wa umoja huo Paul Ntelya alisema kuwa hivi karibuni Baraza la
Madiwani lilitumia zaidi ya shilingi m.40 kwenda kujifunza usafi katika jiji la
Mbeya ambapo niufujaji wa fedha za Serikali.
Aidha Ntelya
alisema wao kama wazee wa mji huo wangeshirikishwa wangewashauri kwenda katika
Jiji la Mwanza ambako napo wangejifunza usafi pia kutokana na mji wa Mwanza
kuwa ni mkubwa na ni msafi hali ambayo wangetumia gharama ndogo.
Alisema
kwamba mji wa Kahama unakua kwa kasi ya ajabu lakini Halmashauri ndiyo
inachangia kuurudisha nyuma mji huo
kimaendeleo badala wajikite katikla kuboresha vyanzo vya mapato kama
Soko kuu linalolalamikiwa kukosa maji,choo pamoja na mifereji ya kupitisha
maji.
‘’Halmashauri
inatuchukia sana sisi Wazee hasa tunaposema matatizo ya mji huu sisi hatulalamikii fedha zinazotumika
bali tunalalamika kuhusu matumizi mabovu katika halmashauri yetu tunashangaa
serikali kutenga kiasi hicho cha fedha milioni 40 kwenda mbali nawengine
kuchukua za kuchezea badala ya kwenda
Mwanza ambapo ni karibu wakaokoa milioni kadhaa.
‘’Wanajifunza
nini hata wakati ule walikwenda Moshi kujifunza huohuo usafi hatujaona elimu waliyoitumia kutoka Moshi
sasa wamechukua mamilioni ya pesa wamekwenda huko Mbeya huku miundo mbinu ya
soko na maeneo mengine ni mibovu wanazidi kuuongezea mji wetu changamoto
rukuki’’Alisema Ntelya.
Kwa upande
wake mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Jidula Mabambasi ambaye pia ni Diwani wa
Kata ya Zongomera akijibu malalamiko hayo alisema kuwa Suala la kwenda Madiwani
wake katika jiji la Mbeya kujifunza Usafi liko kisheria katika Halmashauri zote
za miji.
Alisema
kutokana na hali hiyo malalamiko yao ameyapokea na atayawasilisha katika Baraza
la Madiwani lijalo nakuongeza kuwa siyo wazee tu hata mwananchui wa kawaida
anahaki ya kufuatilia mapato na matumizi katika Halmashauri yao.
No comments: