Afisa Elimu ya msingi halmashauri ya mji Aluko Aluko Akitoa pongezi kwa Bank ya CRDB Wakati wa kukabidhiwa madawat jumla ya madawat( 20) ishirini yenye dhamanu ya shilingi milioni moja na ishirini Elfu
Baadhi ya madawati yalitolewa na Bank ya CRDB ya mjini kahama katika shule ya msingi malunga Ambapo madawati hayo yana dhamani ya shilingi milioni moja na Elf ishilini jumla ya madawati(200)
Mkurugenzi wa Halmashauri ya mji wa kahama Felix kimaryo akitoa pongezi wa meneja wa Bank ya CRDB Mwenye tai nye ufito mweupe kati Luther mneney
Meneja w Bank ya CRDB mjini kahama Luther mneney Akiotoa maelekezo juu ya maendeleo ya shule zetu wachangia madawati kiasi hicho kidogo
Meneja wa CRDB Mwennaye shati nyeupe Akimkabidhi Mkurugenzi wa mji Baadhi ya madawati Ambayo Bank ya CRDB Imetoa kwa shule hiyo ya malunga mjini kahama Ambapo jumla ya madawati 20 nyenye dhamani ya shilingi milioni moja na elfu ishirini
Baadhi ya wanafunzi na mkurugenzi wa halmashauri ya mjin wa kahama ambaya yupo kati ya wanafunzi Felix kimaryo katika shule ya msingi malunga
Baadhi ya Walimu wa shule ya msingi malunga wakiwa na maofisa wa wa Bank ya CRDB Katika picha ya pamoja shuleni hapo
Na Mohab
Dominick
Kahama
May 27, 2014.
CRDB YASAIDIA MADAWATI SHULE YA MSINGI MALUNGA
BENKI ya CRDB Tawi la Kahama Mkoani Shinyanga juzi
ilitoa Msaada wa Madawati 20 yenye thamani ya shilingi milioni moja katika shule ya Msingi ya Malunga Wilayani hapa ili kuwanusuru kundi
kubwa la Wanafunzi wanaosoma katika shule hiyo wakiwa wamekaa chini.
Akitoa Msaada huo katika shule hiyo juzi Meneja wa
CRDB Tawi la Kahama Luther Mneney alisema kuwa Benki yake imeamua kutoa kiasi
kidogo walichonacho ili kuwanusuru Wanafunzi hao baada ya kuletewa ombi na
Mratibu wa Elimu wa Kata hiyo John Tumbo.
Mneney alisema kuwa katika Benki ya CRDB ni kiasi
cha asilimia moja tuu hutolewa kwa ajili ya kusaidia huduma katika jamii na
kiasi hicho hugombaniwa na asasi mbalimbali zinazohitaji misaada hali ambayo
inafanya benki hiyo kuchangia katika sekta tofauti tofauti kila mwaka.
Aidha Meneja huyo alisema kuwa Tatizo la upungufu wa
Madawati katika shule za msingi ni kubwa haliwezi kuisha bila ya kushirikiana wadau mbalimbali ili
kuweza kuwasaidia Wanafunzi ili waweze kutimiza ndoto zao za baadaye
walizojiwekea.
Kwa upande wake Afisa Elimu Msingi wa Halmashauri ya
Mji wa Kahama Aluko Aluko akipokea Madawati hayo alisema kuwa tatizo la
Madawati katika Halmashauri ya Mji wa Kahama ni kubwa na kuongeza kuwa mahitaji
ya Madawati katika shule hizo ni 15,630 wakati kiwango cha madawati yalipo ni
9,320.
Aidha afisa Elimu huyo aliendelea kusema kuwa
kitendo cha Benki ya CRDB kuonyesha nia ya kusadia katika shule hizo ni kitendo
cha kuigwa na Wadau mbalimbali wa Elimu ili kupunguza tatizo hilo na kama sii
kulimaliza kabisa katika Halmashauri hiyo.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa
Kahama Felix Kimaryo alisema kuwa aliwataka Walimu katika shule hiyo ya Msingi
Malunga kuhakikisha kuwa madawati hayo yanatunzwa vizuri ili yaweze kuwasaidia
na wanafunzi wengine ambao watasoma katika shule hiyo.
Alisema kuwa mbali na Benki ya CRDB kutoa msaada
huyo Halmashauri yake Mji pia imetenga bajeti kwa ajili ya kutatua tatizo hilo
la Madawati na hivyo muda sii mrefu hali hiyo ya upungufu wa madawati katika
shule za Msingi katika Halmashuri ya mji wa Kahama litatoweka kabisa.
mwisho
No comments: