sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» »Unlabelled » WAJIFANYA MUNGU WATU KUENDESHA BARAZA LA ARDHI SHINYANGA



Na Mohab Dominick
Shinyanga
May 29,2014,

WAJIFANYA MUNGU WATU KUENDESHA BARAZA LA ARDHI SHINYANGA

Wakazi wa kata ya Tinde katika Wilaya ya Shinyanga Vijijini mkoani humo wamelilalamikia baraza la ardhi la kata hiyo kwa kuwanyima haki zao kutokana na maamuzi ya kesi kutotolewa kwa wakati kwa lengo la kijipatia chochote.

Kauli hiyo imetolewa juzi na mmoja wa wakazi wa kata hiyo,Clement Wiyeke wakati wakizungumza na Waandishi wa Habari kwa nyakati tofauti juu ya baraza hilo kujingeuza kuwa mungu Watu kwa kutowatendea haki  wananchi na kutaka wapewa chochote.

Wiyeke alieleza kuwa wamekuwa hawafanyi kazi kama inavyotakiwa na kwenda kinyume na Sheria ya Mabaraza ya Ardhi ambapo pia wamekuwa wakiangalia ni mtu wa aina ipi aliyepeleka kesi pale kama ni mwenye pesa au la ndipo wamshughuliki swala lake.

 Hata hivyo akiongelea swala hilo mwenyekiti wa baraza la ardhi, Kazumari Mnala Mkulunga alisema kuwa wao kama wasuruhishi wa migogoro ya ardhi katika kata hiyo wanafanya kazi bila kuangalia mtu yeyote mwenyepesa au hana pesa kama inavyodaiwa.

Mwenyekiti huyo alisema wanafanya kazi katika mazingira mangumu kwani hata sehemu ya kuwekea majarada ya kesi hawana bali hujinunulia wao hali ambayo inapelekea kwa baadhi ya mashauri kupotea na kuiomba halmashauri kutowatelekeza kwa shunguli ngumu ambayo haina posho.

Mkulunga ameitaka serikali kuwaboleshea miundombinu na mazingira ya kazi na kuwapatia walinzi kwa shunguli za maamuzi     ya mashauri zinapoendeshwa kutokana na baadhi ya watuhumiwa kuwa wakorofi na wapate ajira ya kudumu kwa wenyeviti pamoja na makatibu kwa kuajiri watu mwenye elimu ya Sheria.

MWISHO.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply