sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» »Unlabelled » KANISA LATOA MSAADA KWA YATIMA NA WAJANE KAHAMA



 Mkuu wa wilaya ya kahama Benson Mpesya Akipokea Baadhi ya Vifaa mbalimbali  toka kwa Baba Askofu Rizik Esrom wa kanisa la huduma mlima wa makimbilio vifaa vya dhamani ya vitu vyote ni milioni 14.5 Msaada huu hulikabidhiwa kwa mkuu wa wilaya ya kahama
 Mkuu wa wilaya ya kahama Benson Mpesya Akiangalia Baadhi ya vifaa vilivyotolewa na kanisa la huduma ya mlima wa makimbilio mjini kahama
 Mkuu wa wilaya ya kahama akiwa na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya na wakuu  wa idara mbalimbali za wilaya ya kahama wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa makabidhiano vifaa mbalimbali toka kanisa la huduma mlima wa makimbilio katika ofisi ya mkuu wa wilaya ya kahama
 Baba Askofu Rizik Esrom Akitoa maelenzo kwa waadishi wa habari katika ofisi ya mkuu wa wilaya ya kahama baada ya kutoa misaada hiyo kwa mkuu wa wilaya ya kahama vifaa hiyo vina dhamani ya milioni 14.5
 Katibu tawala wa ofisi ya mkuu wa wilaya ya kahama mwenye karatasi mkononi julias mushi, kati ni mkuu wa wilaya ya kahama Benson Mpesya mwenye kitabu chekundu ni Baba Askofu Rizik Esrom wa kanisa la huduma mlima wa makimbilio
 Baadhi ya wahuduma ya kanisa la huduma mlima wa makimbilio wakitoa vifaa mbalimbali kwenye magari kwa ajili ya kupelekwa kwa watoto yatima na wajane mjini kahama
 Mmoja wa watumishi wa ofisi ya mkuu wa wilaya ya kahama alitambulika kwa jina moja tu la ungumba akisaidia moja ya mzingo iliyoletwa na kanisa la huduma la mlima  makimbilio
 Baadhi ni vifaa vya msaada toka kanisa la huduma mlima wa makimbilio vikiwa katika ofisi ya mkuu wa wilaya kahama leo


Na  Mohab Dominick
Kahama
May 29, 2014.

KANISA LATOA MSAADA KWA YATIMA NA WAJANE KAHAMA

ASKOFU wa Kanisa Huduma Mlima wa Makimbilio Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga Rizik Esrom juzi alitoa Msaada  wa Nguo kwa Serikali ya Wilaya ya Kahama kwa lengo la kusaidia akinamama wajane na Watoto Yatima waliopo Wilayani hapa.

Akitoa Msaada huo kwa Mkuu wa Wilaya ya Kahama Benson Mpesya, Askofu huyo alisema kuwa Kanisa lake limeguswa na kutoa msaada huo na kuona ni muhimu sasa katika kuwatazama Mayatima na Wajane waliopo Wilayani hapa.

Esrom alisema kuwa msaada huo pia umelenga Akinamama wajane wasiokuwa na uwezo kabisa wa kufanya kazi hali ambayo itapunguza ugumu wa maisha walionayo katika familia wanazoishi.

Askofu huyo alisema kuwa msaada huo una jumla ya thamani ya milioni 14.5 na kuongeza kanisa lake halitaishia hapo katika kuchangia kwa jamii isiyojiweza katika Wilaya ya Kahama na kuongeza  kuwa huo ni mwanzo tuu.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kahama Benson Mpesya akipokea msaada huo kwa niaba ya Serikali alisema kuwa msaada huo umekuja wakati muafaka na kuongeza kuwa atawaita Maafisa wa Maendeleo ya jamii katika Halmashauri tatu ili waweze kuona jinsi ya kuzigawa katika maeneo yao.

Mpesya aliwataka Makanisa mengine Wilayani hapa kuguswa kama lilivyoguswa kanisa hilo katika kusadia katika shughuli za maendeleo ya jamii hususani katika kuchangia watu wasiokuwa na uwezo kama Watoto Yatima pamoja na Wajane.

Aidha alisema kutoa ni moyo na sio utajiri na watu wa aina hiyo ni muhimu katika kuwasaidia ili na wao wajione kama watu wengine na sii kuwaacha wapweke huku wakijua kuwa hawana msaada wowote katika jamii inayowazunguka.

mwisho

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply