sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» »Unlabelled » AFARIKI DUNIA KWA KUGONGWA NA ROLI KAHAMA





Na  Mohab Dominick
Kahama
Juni 24,2014

AFARIKI DUNIA KWA KUGONGWA NA ROLI KAHAMA

MTU mmoja Mkazi wa Kahama Mkoa wa Shinyanga Mwenyeasili ya Kihindi Ismail Mohamed Walu amefariki Dunia kwa kugongwa na Roli aina ya Fuso linalosomba mchanga lenye namba za usajili  T161 AQR mali ya Ndeleye Mkazi wa Kigoma.

Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Shinyanga Kihenya kihenya alithibitisha kupokea kwa taarifa hizo na kuongeza Tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa tisa mchana wakati Mohamed akiwa anaendesha baiskeli akitokea bijampola kueleke Kahama mjini ndipo Gari hilo lilimgonga na kupoteza maisha hapohapo likiwa liaelekea Shunu.

Kamanda Kihenya alisema kuwa Chanzo cha ajali ni Mwendokasi aliokuwanao Dereva wa Roli hilo na alipomgonga marehemu huyo alilitelekeza Gari hilo na kwenda kusikojulikana na jeshi la Polisi mkoani humo linaendelea na jitihada za kumsaka Dereva huyo.

Hata hivyo Wananchi waliokuwa kwenye tukio hilo walisema Jeshi la usalama Barabarani Wilayani  humo limeshindwa kuyaondoa maroli Makubwa ambayo yanaegeshwa pembezoni mwa Barabara hizo ambapo yamekuwa yakisababisha ajali mara kwa mara kutokana na kuibana njia.

mwisho

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply