sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» »Unlabelled » MUUGUZI MMOJA ANUSURIKA KIFUNGO KWA KUTELEKEZA FAMILIA





  

Na  Mohab Dominick
Kahama,
Juni 24,2014


Muuguzi mmoja Juma Deo (29) wa  Zahanati ya Bakwata Wilayani Kahama mkoani Shinyanga ambaye ni mkazi wa Maswa Mkoani Simiyu, amenusurika kufikishwa mahakamani kwa tuhuma za kutelekeza mke na watoto wawili kwa madai ya kutompenda mke wake.

Sakata hilo limetokea mwishoni wa juma lililopita katika Ofisi ya Maendeleo ya Jamii ya Halmashauri ya Mji wa Kahama kufuatia malalamiko yaliyofunguliwa na Veronika John(21) mke wa Deo mwenye watoto wawili mmoja wa miaka minne na mwingine mwaka mmoja.

 Afisa Ustawi wa Jamii wa Halmashauri ya Mji wa Kahama Regina Nkwabi alisema  kuwa Ofisi yake ilipokea malalamiko kutoka kwa Veronika kabla ya kumwita Deo na kuwatambua watoto wake aliowatelekeza pamoja na Mama yao.

 Nkwabi alisema Ofisi yake ilipewa uwezo wa kumshauri mume anapotelekeza watoto aweze kuwahudumia, na kwamba akikataa hufikishwa mahakamani ambapo faini yake ni shilingi 5,000,000 au kwenda jela miezi sita; au vyote kwa pamoja.

Veronika alikaa kwa wazazi wa Deo huko Maswa wakati wote Deo alipokuwa akisoma katika Chuo cha uuguzi (PHN) cha mjini Kahama, na alipoajiriwa hakurudi tena kwa mkewe hadi wazazi wa deo walipomfukuza Regina na watoto wake.

Alipotakiwa kueleza sababu ya kutohudumia watoto wake, Deo alisema alishindwa kutuma pesa kwa kuhofia Veronica angetumia vibaya fedha hizo huku akiwa nauamuzi wa kuachana naye kwa kuwa ni mbishi, na kwamba tayari alipata mchumba mwingine wilayani Kahama.

 Kufuatia maelezo hayo Ofisi ya Usatawi wa Jamii ilimwamuru Deo kuweka mkataba wa kumpangishia nyumba ya kuishi Veronika na watoto wake, kutoa mahitaji ya kila siku na kumwanzishia Regina mradi ili aweze kujitegemea kiuchumi.

Tukio hilo lilitokea siku chache tu tangu Kauli ya Mkuu wa Wilaya ya Kahama Benson Mpesya kuwaagiza watendaji wa Kata kuwashughulikia wanaume wanaolalamikiwa na wanawake waliozaa nao kutelekeza watoto wakilelewa na mama zao peke yao. mwisho

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply