sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» » SERIKALI KAHAMA KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA MIGODI


SERIKALI Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga kwa kushirikiana na Mgodi wa Barrick Buzwagi imesema kuwa watakuwa mstari wa Mbele katika kuhakikisha wanawaunganisha Vijana kupitia masula ya Michezo ili kuhakikisha kuwa Wilaya ya Kahama inakuwa mstari wa mbele katika sekta nzima  ya Burudani na Michezo.

Mkuu wa Wilaya ya Kahama Benson Mpesya aliyasema hayo wakati akifunga Bonanzala siku tatu lililoandaiwa na Kampuni ya Mgodi wa Dhahabu wa African Barrick Gold (ABG) Kupitia Mgodi wa Buzwagi  kwa lengo la kuwaunganisha Vijana ikiwa ni sambamba na kufahamiana.

Lengo lingine kusherekea ufungwaji wa Mashindano ya Kombe la Dunia yalikuwa yakionyeshwa na Kampuni hiyo kupitia senema katika uwanja wa Halmashauri hali iliyochangia Wananchi kuangalia mashindano hayo kwa muda wamwezi mzima bila ya kutoa gharama yeyote.

Alisema kuwa kwa Serikali Wilayani hapa kwa kushirikiana na wawekezaji hao na kuhakikisha kuwa Wilaya ya Kahama inakuwa na kusonga mbele katika masuala ya michezo hususani Mpira wa Miguu ambao umepoteza mwelekeo tangu iliposhuka daraja timu ya Kahama united.

Alisema kuwa Serikali inatambua uwepo wa wawekezaji katika Wilaya ya Kahama na kuongeza kuwa wataendelea kushirikiana katika masuala mbalimbali ikiwa ni sambamba na michezo ili kuinua vipaji kwa wakazi wa mji wa Kahama.

“Msi waogope wawekezaji kwani wao sio Wanyama ni binadamu kama sisi tushirikiane ili tukuze michezo katika Mji wetu ambao kwa sasa unakuwa kwa kasi na tunatakiwa kuwa ni timu katika ligi kuu huko tuendako”, Alisema Benson Mpesya Mkuu wa Wilaya ya Kahama.

Kwa upande wake Kaimu Meneja Mkuu wa Mgodi wa Buzwagi (ABG) Amos John alisema kuwa Kampuni yake itaendelea kutoa ushirikiano kwa vijana wa Mji wa Kahama na kuongeza kuwa wapo tayari katika kuhakikisha wananchi wa Kahama wanajenga mahusiano mazuri na Mgodi


Na  Mohab Dominick-Kahama

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply