sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» » » WANANCHI ISONDA WATAKIWA KUWEKA MAHUSIANO MAZURI NA WAWEKEZAJI.

 Hili ndiyo eneo la mgodi wa vasista mines katika kijiji cha isonda wilayani nyanghwale mkoani Geita .
 Mwenye kipasa sauti ni meneja mradi wa kampuni ya vasista Goodluk kafutila na mgeni rasmi mkuu wa wilaya ya nyanghwale Ibrahimu marwa wakati wa kuweka jiwe la msingi katika mgodi huu .
 Mkuu wa wilaya ya nyanghwale ibrahumu marwa ambaye anapinga makofi  karibu sana katika mgodi wetu wa vasista mines .
 Mkurungezi wa vasista mines Bhavan Rajesh akitoa neno kwa mkuu wa wilaya ya nyangwale njisi mgodi huu hutakapotoa huduma kwa mwanachi wa kijiji cha isonda wilaya hapa .
 Meneja mradi Goodluck kafutila mwenye shart nyeusi akisalimiana na mkuu wa wilaya ya nyanghwale mwenye shati nyeupe ni mkurungezi Bhavan Rajesh wakati mkuu huyo wa kuweke jiwe la msingi
 Mkurungezi wa mgodi wa visista mines Bhavan Rajesh wakati akitoa hotuba kwa mgeni rasmi
 Wangeni walikwa wa kijiji cha isonda kata ya nyungwa wilayani nyanghwale .

 Baadhi ya wakurungezi wa mgodi wa vasista wakiwa wanangalia usalama eneo hilo
 Askari wa ulinzi wakiwa katika mkakati wa  ulinzi wa kampuni  visista mgodi huo .
 Wafanyakazi wa mgodi wa visista wakiwa katika shughuli zao za madharizi ya mgeni rasmi mkuu wa wilaya ya nyanghwale.
 Mkuu wa wilaya ya nyanghwale Ibrahimu marwa akipewa maelenzo na meneja mradi goodluck kafutila
 Mkuu wa wilaya ya nyanghwale akiwa katika picha ya pamoja na wana kijiji cha isonda wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi wa mgodi huu .
 Mwenye sharti ya rangi ya maziwa kati wa nne mkuu wa wilaya ya nyanghwale Ibrahimu marwa akiwa picha ya pamoja na uongozi wa mgodi wa vasista mines mwenye sharti nyeusi ni meneja mradi goodluck kafutila .
 Mwenye kuonyesha mkono ni meneja mradi wa mgodi wa vasista mines maeneo ya mgodi huu
 Baadhi ya majengo ya ofisi za vasista mines katika kijiji cha isonda
 Pia mapochopocho yalikuwepo bana wewe wacha tu hii ni habari nyingine
 Huu ni mtambo mdogo wa uchenjuaji wa dhahabu wa bila kutumia madawa .
 Wafanyakazi poa tu
 Burundani kwa wazee wa kijiji cha  isonda baada ya kuweka jiwe la msingi na mkuu wa wilaya ya nyanghwale Ibrahimu marwa .
 Baadhi ya wakurungezi na watumishi wa vasista mines wakijadiliana juu ya mambo yalivyokwenda wakati wa uzinduzi huu.

 Pia utunzaji wa mazingira upo kama jinsi vitalu vya miche vikiwa vimeoteshwa
 Mkurungezi wa mradi katika mgodi wa vasista mines  Goodluck kafutila akitoa neno la shukurani kwa mgeni rasmi .
Mkuu wa wilaya ya nyanghwale Ibrahimu marwa akiutubia wanachi wa kijiji cha isonda hawapo pichani wakati wa kuweka jiwe la msingi mgodi hapa .



Na Mohab Dominick
Nyang’hwale
Agust 7 , 2014.

WANANCHI wa Kijiji cha Isonda Kata ya Nyugwa Wilayani Nyang’wale Mkoani Geita wametakiwa kujenga mahusiano mazuri na Wawekezaji waliopo katika Kijiji hicho kwa lengo la kufaidika na huduma mbalimbalimbali za kijamii ili kuharakisha  maendeleo yao.

Diwani wa Kata hiyo Donard Kaboroso aliyasema hayo juzi wakati wa uwekaji wa jiwe za msingi wa Mwekezaji kutoka India kampuni ya Vasista itakayo juhusisha na uchenjua wa  Madini ya Dhahabu katika katika kijiji cha Isonda.

Kaboroso alisema kuwa Wananchi wa Isonda wakiwa na mahusiano mazuri na Mwekezaji huyo wanaweza kupata faida nyingi hasa katika mambo mbalimbali ya Kijamii kama vile Elimu Afya hali ambayo itaweza kuleta mabaliko makubwa katika Kijiji hicho na Wilaya ya Nyang’wale kwa ujumla.

Nae Meneja Mradi wa Mradi wa Kampuni ya Vasista Goodluck Kafutila akisoma Taarifa ya ujenzi wa Mgodi huo mbele ya Mgeni Rasmi katika uzinduzi huo Mkuu wa Wilaya ya Nyang’wale Ibrahimu Marwa alisema kuwa Kampuni ya Vasista imeingia ubia na waafrika na kuongeza kuwa Mgodi huo pia utafanya kazi bila ya kutumia Kemikali.

Kafutila alisema kuwa Mgodi huo ambao unategemea kukamilika ujenzi wake mwezi desemba mwaka huu utatoa ajira kwa wataalamu mbalimbali wa madini wazawa na kuongeza kuwa jumla wafanyakazi zaidi ya 100 watapata ajira kupitia mgodi huo ikiwa ni pamoja na wakazi wa Vijiji vya jirani.

Pia alisema kuwa mbali na ajira pia Mgodi huo pia utasaidia katika Wanakijiji wa Isonda katika sekta za Kilimo cha umwagiliaji maji, umeme wa mionzi ya jua pamoja na kutoa Elimu ya utunzaji wa mazingira kwa watu wa Kijiji hicho hali ambayo italeta mabadiliko kuliko ilivyokuwa hapo awali.

Alisema kuwa faida nyingine watakayaopata wanakijiji wa Kijiji hicho ni pamoja na kupata fura kubwa ya kuuza bidhaa zao katika Mgodi huo kama vile mbogamboga ambazo zitakazokuwa zikilimwa katika eneo hilo hali ambayo itakuza kipato cha mtu mmoja mmoja katika eneo hilo na kuleta mabadiliko.

Aidha Kafutila alisema kuwa Mgodi huo wa Vasista utakuwa na uwezo wa kusindika tani 10 za udongo kwa saa ikiwa ni sawa na tani 140 za udongo kwa siku kiasi ambacho ni kikubwa kulinganisha na uwezo wa uzalishaji wa Mgodi huo.

Kwa upande wake Mgeni Rasmi katika uzinduzi huo Mkuu wa Wilaya ya Nyang’wale Ibrahimu Marwa alisema kuwa kazi kubwa ya Serikali ni pamoja na kuhakikisha inaweka mazingira mazuri kwa wawekezaji hapa nchini ili watanzania waweze kunufaika na rasilimali zao zinazowanguka katika maeneo yao.

Mwisho.



«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply