sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» » » JESHI LA POLISI KAHAMA WAOMBA UHUSHIRIKIANO NA WANANCHI SIKU ZA SIKUKU YA MWAKA KRISMAS NA MWAKA MPYA

 Nembo ya jeshi la polisi
 Baadhi ya askari  wa kituo cha polisi wilayani kahama wakiwa katika barabara kuu ya maeneo ambayo yanasemekana kuwa na fujo katika sherehe hizi za sikuku wakiwa tayari kwa lolote lile.


Jeshi la polisi wilayani Kahama mkoani Shinyanga limetoa wito kwa wananchi wilayani humo kutoa ushirikiano na jeshi hilo kwa kutoa taarifa za uhaarifu ili kuimalisha ulinzi na usalama kuelekea katika sikukuu za krismasi na mwaka mpya.

Mkuu wa kituo cha polisi wilayani Kahama Elias Ulomi alisema kuwa wananchi wanawajibu wa kushirikiana na jeshi la polisi katika kulinda amani na utulivu katika kipindi hiki cha msimu wa sikuu za krismasi na mwaka mpya kwa kutoa taarifa ya vyanzo vyote vya uharifu  kama wizi na uporaji wa mali zao.

Ulomi amesema kua jeshi la polisi wilayani humo limejipanga vyema kuhakikisha amani na utulivu kwa wananchi wake kuelekea katika sikukuu hizo ambapo jeshi hilo limeweka mipango madhubuti ya kuimalisha ulinzi na usalama hasa katika maeneo yote ya kumbi za starehe kama baa,na klabu, ambapo kutakuwa na walinzi wakutosha kuanzia siku ya mkesha wa krismasi na kuendela hadi sikuu ya mwaka mpya.

Ameongeza kuwa katika kipindi hiki cha sikukuu kumekuwepo na matukio mbalimbali kama ajari za barabarani pamoja na baadhi ya wananchi katika maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo kuvamiwa na kupolwa malizao na hivyo kuwaomba wananchi wote kuwa waangalifu  katika kipindi hiki ili waweze kusheherekea sikukuu hizo kwa amani na utulivu.

“jeshi la polisi tumejipanga vizuri na niwatoe hofu wananchi wote  wilayani Kahama washeherekee kwa amani na uhuru  siku ya sikukuu kwani ulinzi utakuwepo wa kutosha katika maeneo yote,nawatakia sikukuu njema na mungu awabariki”alisema Ulomi.

Sikukuu ya krisimasi huadhimishwa Decemba 25 kila mwaka ambayo ni sikukuu ya kiimani kwa wakristo wote duniani kuadhimisha siku ya kuzaliwa kwa mwokozi Yesu kristo,hali kadharika sikukuu ya mwaka mpya huadhimishwa januari mosi kila mwaka ikiwa ni mwanzo wa mwaka mpya .
mwisho



«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply