sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» » » PESA ZA ESCROW SI ZA UMMA,ASEMA RAISI KIKWETE



Prof. Anna Tibaijuka aliyeng'olewa uwaziri jioni hii nchini Tanzania.Unakumbuka wiki iliyopita Waziri Anna Tibaijuka alijitapa kuwa akijiuzulu hata Rais Kikwete atamshangaaa? Lakini cha ajabu leo Rais Kikwete amemtaka atoke kwenye nafasi hiyo ya Uwaziri na achaguliwe mtu mwingine.

Akiwa kama Mtumishi wa serikali ambaye anatakiwa kufuata maadili ya Utumishi  wa umma  aliamua kupokea kiasi kikubwa cha fedha huku akijua kimaadili kama mtumishi wa serikali haitakiwi, Rais Dr. Jakaya Kikwete amesema hayo wakati  akizungumza na taifa kupitia Wazee wa Dar es Salaam leo katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.

Kwa upande wa Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo na Katibu Mkuu wa Wiazara hiyo Eliackhim  Maswi  amesema ameagiza uchunguzi ufanyika na katika muda wa siku mbili au tatu hivi atapewa taarifa ya uchunguzi huo na kuchukua hatua stahiki.

Na Kwa upande wa Majaji wa Mahakama Kuu waliotuhumiwa Rais Dr. Jakaya Kikwete amesema anamwachia Jaji Mkuu Mh. Jaji Mohammed Chande Othman ili achukue hatua za kimaadili kutokana na taratibu za kimahamama na mara baada ya kujiridhisha atapewa taarifa na Jaji mkuu na kuchukua hatua.



«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply