sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» » WATOTO 18 WAZARIWA KWENYE MKESHA WA CHRISTMAS KAHAMA

Baadhi ya watoto walizaliwa usiku wa mkesha wa chritsmas katika hospitali ya wilaya ya kahama .

JUMLA ya watoto kumi na nane wamezaliwa usiku wa mkesha wa sikukuu ya Christmas katika hospitali ya wilaya ya Kahama mkoani shinyanga ambapo kati ya hao 10 niwakiume na wakike 8.

Akizungumza  mganga mfawidhi hospital ya wilaya ya Kahama Dkr,Charles Rwaikeza,alisema kuwa jumla ya watoto kumi na nane wamezaliwa usiku wa mkesha wa sikuku ya Christmas wote wakiwa wamezaliwa salaama bila matatizo yoyote.

Alisema kuwa alipokea takwimu za watoto waliozaliwa kutoka kwa wakunga waliokuwa zamu ambapo ilikuwa jumla ya watoto kumi nane wamezaliwa wakiwa na afya njema ambapo watoto wakike 8 pamoja na watoto wakiume walikuwa ni 10.

Hata hivyo Rwaikeza amewataka wakinamama waepuke kujifungulia nyumbani badala yake pindi wanapojihisi mabadiliko ya kimwili wakati wa ujauzito wawahi katika hospital ama zahati zilizo karibu nao ili kupata matibu ikiwa ni njia mojawapo ya kujifungua salaama.

Aliongeza kuwa pindi wakimama wajawazito wanapokuwa hospitalini wakisubili wakati wa kujifungua na kupata usumbufu kutoka kwa wauguzi wasisite kufika katika ofsi ya mganga mfawidhi kwa lengo la kupatiwa ufumbuzi wa matatizo yanayokuwa yamejitokeza kwa wauguzi wa zamu.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply